<?xml version='1.0' encoding='UTF-8'?><?xml-stylesheet href="http://www.blogger.com/styles/atom.css" type="text/css"?><feed xmlns='http://www.w3.org/2005/Atom' xmlns:openSearch='http://a9.com/-/spec/opensearchrss/1.0/' xmlns:georss='http://www.georss.org/georss' xmlns:gd='http://schemas.google.com/g/2005' xmlns:thr='http://purl.org/syndication/thread/1.0'><id>tag:blogger.com,1999:blog-6014809184859864743</id><updated>2012-02-16T09:12:28.965-08:00</updated><title type='text'>FALSAFA YA UTU NA ITIKADI YA HAKI</title><subtitle type='html'></subtitle><link rel='http://schemas.google.com/g/2005#feed' type='application/atom+xml' href='http://georgekahangwa.blogspot.com/feeds/posts/default'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/6014809184859864743/posts/default?max-results=100'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://georgekahangwa.blogspot.com/'/><link rel='hub' href='http://pubsubhubbub.appspot.com/'/><author><name>Kahangwa</name><uri>http://www.blogger.com/profile/07414631690002879283</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='32' height='24' src='http://bp3.blogger.com/_3R2qky2qHsg/R9AwRuFfYjI/AAAAAAAAAAM/4OhJy7kgqsE/S220/george.jpg'/></author><generator version='7.00' uri='http://www.blogger.com'>Blogger</generator><openSearch:totalResults>8</openSearch:totalResults><openSearch:startIndex>1</openSearch:startIndex><openSearch:itemsPerPage>100</openSearch:itemsPerPage><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-6014809184859864743.post-6047497003795599251</id><published>2010-05-12T06:23:00.000-07:00</published><updated>2010-05-12T06:24:16.518-07:00</updated><title type='text'>NAFASI YA KUFANYA MABADILIKO 2010</title><content type='html'>Ndugu zangu watanzania,&lt;br /&gt;Mbele yetu ipo nafasi ya kufanya maamuzi nyeti juu ya mustakabari wa taifa letu na juu ya mustakabari wa kila raia wa taifa hili. Tunayo nafasi nyingine mwaka huu, ya kuuondoa katika atamu mfumo ambao umeiharibu nchi kwa kuendelea kuwanufaisha watu kadhaa wachache na kuwaacha mamilioni ya watanzania katika dhiki zisizomithirika. Tunayo nafasi sasa ya kumaua kwamba taifa letu linaweza kuwa na uchumi imara kabisa na hivyo kutufanya tuondoke katika aibu ya umaskini ambayo tumedumu nayo kwa miaka mingi.&lt;br /&gt;Fursa iko mbele yetu ya kuamua kwamba zile adha za kupata huduma mbovu za afya katika mahospitali yetu, elimu duni katika mashule yetu, miundombinu hafifu katika nchi yetu, sasa mwisho wake umewadia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa zaidi ya miongo minne, tumekuwa na utawala ulio mwapesi kutulaghai kwa kutuahidi kwamba utatupatia maisha bora kila mmoja wetu, kwamba unafanya jitihada za kuondoa kero za wananchi. Sote ni mashahidi kwamba ahadi zao zimegeuka kuwa uongo ama kwa sababu tokea awali walikusudia kutudanganya ili wajinufaishe wenyewe, au uwezo wao wa kushughulikia masuala haya ama kwa hakika ni mdogo.&lt;br /&gt;Tunayo mamlaka ya kumwambia mwongo ya kwamba uongo wake sasa basi. Mbele yetu ni fursa ya kuthibitisha kwa vitendo kwamba hatuko tayari tena kumpa nafasi nyingine mtu yeyote aliyeshindwa kuishi maneno yake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa uamuzi tutakaoufanya mwezi Oktoba, tunaweza kabisa kuifanyia mabadiliko makubwa sana nchi yetu ili kuleta tija katika kila sekta na hatimaye tuwe na taifa lenye nguvu za kiuchumi na maendeleo ya haja.&lt;br /&gt;Hata lini tutalia kwamba katika hospitali zetu wagonjwa wanalala ‘mzungu wa nne’ na hakuna dawa. Asiyetaka kusikiliza kilio hiki tunamfahamu tayari.&lt;br /&gt;Hata lini tutalalamika kwamba elimu imekuwa duni, shule hazina walimu, na tuna mitaala isiyoridhisha.  waliotufikisha hapo mbona tunawajua kwa majina.&lt;br /&gt;Hata lini tutanungumika kwamba mwananchi wa kawaida hafaidishwi na uchumi wan chi, bali wageni na wenye nacho tayari. Aliyecheza hii kamali mbona tunamfahamu.&lt;br /&gt;Hata lini tutastaajabia kuona watawala wakiishi kwa anasa na starehe ilihali wananchi wakitaabika katika dhiki. Waliojenga utaratibu huu, na wasikuwa tayari kuona unabadilika tunawamanya.&lt;br /&gt;Ni nani basi awe ‘Yuda’ wa taifa letu kwa mwaka huu hata aendelee kutumia kura yake kuwapa mafisadi hatamu za utawala? Tafadhali, sio wewe msomaji.&lt;br /&gt;Ni nani basi awe mzalendo wa kweli kwa taifa letu hata atumie upigaji kura wake kulibadilisha Taifa. Naam, unao uamuzi, jiunge na wenye nia hiyo.&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/6014809184859864743-6047497003795599251?l=georgekahangwa.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://georgekahangwa.blogspot.com/feeds/6047497003795599251/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=6014809184859864743&amp;postID=6047497003795599251' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/6014809184859864743/posts/default/6047497003795599251'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/6014809184859864743/posts/default/6047497003795599251'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://georgekahangwa.blogspot.com/2010/05/nafasi-ya-kufanya-mabadiliko-2010.html' title='NAFASI YA KUFANYA MABADILIKO 2010'/><author><name>Kahangwa</name><uri>http://www.blogger.com/profile/07414631690002879283</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='32' height='24' src='http://bp3.blogger.com/_3R2qky2qHsg/R9AwRuFfYjI/AAAAAAAAAAM/4OhJy7kgqsE/S220/george.jpg'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-6014809184859864743.post-625663316363467970</id><published>2010-01-04T08:00:00.000-08:00</published><updated>2010-01-04T08:01:38.839-08:00</updated><title type='text'>MOJAWAPO YA SIRI ZA SIASA</title><content type='html'>Mara kadhaa nimealikwa katika makongamano ya vijana kuzungumzia kwa mfano nafasi ya vijana katika siasa. Kutokana na yale tuliyofunzwa shululeni kuhusu uandishi wa mada za kuwasilisha (presentation) nilijikuta mara zote nikiingiza ainisho la neno siasa katika utangulizi wa mawasilisho yangu. Nakumbuka mwaka fulani katika ukumbi wa shule ya sekondari ya Perfect Vision ya jijini Dar es Salaam, niliiambia hadhira mbele yangu hivi; Siasa maana yake ni njia azitumiazo mtu au kundi la watu kupata nguvu na madaraka, na ikitokea mtu akapata nguvu hizo huendelea na hatua ya pili ya njia hizo ili kuhahihisha anabaki na nguvu zake au na madaraka yake kwa lengo la kuendelea kufanya kile alichokikusudia. Kinachogomba hapo ni nguvu azipatazo mwanasiasa anazitumia kwa maslahi ya nani.&lt;br /&gt;Baada ya mawasilisho niliulizwa masawali kadhaa, mengi yakihusu msingi wa mada yaani vijana na nafasi yao katika huo utafutaji na utumiaji wa nguvu. Wakati wa chai, alinifuata kijana mmoja akaniuliza hivi; ‘kumbe mwenzetu uko katika siasa, nini siri ya urembo?’ kwa kuwa aliuliza swali kiutani, niliishia kumjibu (pengine bila kutafakari sana); ‘sio siri, ni kuamua tu’. Tuliishia kucheka na hatimaye chai ikawa imeisha, kuashiria mwisho wa kongamano, maana kabla ya chai vikumbo vya kumwona mwekahazina na wasaidizi wake vilikuwa vimeishapigwa.&lt;br /&gt;Leo hii ninapotizama nyuma, ninawiwa kutafakari, nini siri ya mtu kuwepo katika siasa, kwa maneno mafupi nini siri ya siasa. Majibu yanaweza kuwa mengi, lakini leo nataka kuwashirikisha jibu hili, ambalo naamini kwa hakika linadokeza siri hasa ya siasa.&lt;br /&gt;Jamii nyingi duniani zimegawanyika kiuchumi katika makundi mawili, yaani wenye uwezo kiuchumi na wasio na uwezo huo. Yawezekana kukawa na kundi la katikati, lile la wenye uwezo wa wastani. Misemo mingi imekuwa ikitumika kuyaeleza makundi haya, matharani; wenyenacho na wasionacho, au walalaheri na walalahoi. Kila moja la makundi haya lina maslahi yake katika uchumi ambayo hayana budi kulindwa au kutetewa. Wenyenacho wanatamani kisiwaondokee na ikiwezekana wapate zaidi. Wakati huo huo wasionacho wanataka wapate na jitihada zao zisiishie kufyonzwa na wenyenacho. Kwa ufupi hayo ndio maslahi ya makundi haya. Ni katika jitihada za kulinda maslahi, linapojitokeza kundi la watu (yamkini wajanja wajanja hivi) wakiuomba umma uwape nguvu za kutetea maslahi.&lt;br /&gt;Ukichukulia mfano wa mechi ya mpira wa miguu, timu ya walionacho dhidi ya timu ya wasionacho, marefa, makamisaa na chama cha mpira ndio hao waamuzi wa mechi. Mambo yanaweza kwenda vyema kama waamuzi hawa watahakikisha ‘fair play’ tu ndio inakuwa sheria-mama ya mchezo. Lakini imetokea mara nyingi kwamba marefa wameionea timu fulani na kuipendelea timu nyingine.&lt;br /&gt;Ninachomaanisha hapa, mwanasiasa ni refa wa kiuchumi katika jamii. Siri yake ni maslahi anayoyapata kutokana na kazi yake hiyo, na ili apate maslahi yake inategemea analinda maslahi ya nani. Mwanasiasa anaweza kuamua kulinda maslahi ya walionacho, mwingine anaweza kuamua kuwa mlinzi wa maslahi ya wasionacho, na mwingine akatetea maslahi ya pande zote mbili (au tuseme pande tatu, maana na yeye ana maslahi yake)&lt;br /&gt;Tukiziangalia siasa za Afrika (waweza kusema za Tanzania) za wakati huu, kwa mtazamo wangu, wanasiasa walioko madarakani  ni watetezi na walinzi wa maslahi ya mwenyenacho. Kwa kufanya hivyo nao wananufaika. Katika utetezi wao huo wamekuwa wakiambatanisha unafiki kwa kujifanya wanatetea maslahi ya wasionacho  kwa kuwagawia viperemende ndani ya karatasi za plastiki.&lt;br /&gt;Wakati huo huo kuna wanasiasa waliopewa jina la wapinzani. Hawa nao kwa kauli zao (nasisitiza; kwa kauli) wanajitahidi kuonekana wanatetea maslahi ya wasionacho, ingawa wengi wa wasinacho wanaelekea kutoelewa bado ni nini hasa hawa watetezi ‘wapya’ wanakimaanisha. Pengine wanajiuliza kwamba, hawa wapinzani kinachowasukuma ni mapenzi yao kwa wasionacho au na wao wanatafuta nafasi ya kuwa karibu na mwenyenacho ili wafaidi? Wasionacho wanaendelea kujiuliza, vipi hao wachache toka upinzani ambao tumewasikiliza, wakapenya hadi kwenye viti vya madaraka na nguvu, wamekuwa watetezi wenye tabia gani?&lt;br /&gt;Wanasiasa upenda kuoa ushaidi wa utetezi wao wa maslahi kwa alama ya mambo yaliyofanyika kwa jitihada zao, matharani miundombinu iliyojengwa, huduma za jamii na kadhalika. Ndugu msomaji, haijengwi barabara pasina kulengwa maslahi ya kundi. Barabara inaweza kujengwa ili mwenyenacho aufikie mzinga wa asali na kuirina kisawasawa. Lakini mwanasiasa kwa ulaghai wake atasimama na kuwambia wasionacho; jamani nimewajengea barabara ya lami. Wasionacho huenda wasione kwamba hiyo barabara badala ya kunufaika nayo, ndio kwanza inatumika kama mrija wa kufyonza kisima cha raslimali hadi kikauke. Mwigine atasimama na kusema; nipeni muhula wa pili nimejenga au nimepanua ‘intaneshono eapoti’ (uwanja wa ndege). Ni vyema umma ukaacha kushangilia tu upanuzi bila kujiuliza na kutathmini kwa kina upanuzi huo ni kwa maslahi ya nani. Yasije yakawa ni yale yale, ije midege isombe kila samaki na kutuachia mapanki, harafu ushuru wa mijidege uingizwe kwenye akaunti za wanasiasa.&lt;br /&gt;Mara nyingi hata mimi huwa najiuliza ninaposikia hili neno miundombinu; mbinu za nani? Huwa najiuliza pia, serikali bora ni ipi; inayojenga nyumba za wafanyakazi au inayojenga (inayosaidia kujenga) za wakazi? Mnh, ajengaye za wafanyakazi anataka wawe karibu na eneo la kunyonyewa nguvu kazi zao kwa maslahi ya mwajiri kisha wakistaafu ‘watajiju’, bali ajengaje za wakazi anaitakia jamii maisha bora ujanani na uzeeni.&lt;br /&gt;Ndugu zangu, kwa siri hii niliyowashirikisha, natoa changamoto ya kuendelea kutafakari sera za kiuchumi za wanasiasa dhidi ya maslahi. Unaposikia sera kama; kuvutia wawekezaji, ubinafsishaji, uchangiaji huduma na nyinginezo, unaona ndaniye maslahi ya nani.&lt;br /&gt;Siri ya siasa; ulinzi wa maslahi ya kundi ili mwanasiasa naye apate chake. Maslahi ya nani yanalindwa na mwanasiasa husika ndio yanayowatofautisha wanasiasa wetu. Kazi yetu kujua tunamchagua yupi. Angalizo; miongoni mwa wanasiasa, wapo wachache sana ambao wanatoa kafara maslahi yao wenyewe kwa ajili ya kulinda tu maslahi ya kundi wanachagua kulitumikia, yamkini hao ndio walio bora.&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/6014809184859864743-625663316363467970?l=georgekahangwa.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://georgekahangwa.blogspot.com/feeds/625663316363467970/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=6014809184859864743&amp;postID=625663316363467970' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/6014809184859864743/posts/default/625663316363467970'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/6014809184859864743/posts/default/625663316363467970'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://georgekahangwa.blogspot.com/2010/01/mojawapo-ya-siri-za-siasa.html' title='MOJAWAPO YA SIRI ZA SIASA'/><author><name>Kahangwa</name><uri>http://www.blogger.com/profile/07414631690002879283</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='32' height='24' src='http://bp3.blogger.com/_3R2qky2qHsg/R9AwRuFfYjI/AAAAAAAAAAM/4OhJy7kgqsE/S220/george.jpg'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-6014809184859864743.post-8057906705033401966</id><published>2009-05-27T06:38:00.000-07:00</published><updated>2009-05-27T06:40:56.642-07:00</updated><title type='text'>ITIKADI NA MUSTAKABARI WA TAIFA</title><content type='html'>&lt;div align="justify"&gt;&lt;strong&gt;NAFASI YA ITIKADI KISIASA KATIKA MUSTAKABALI WA TAIFA&lt;br /&gt;&lt;/strong&gt;Mustakabali wa taifa unategemea sana utendaji wa wanataifa na wadau wao katika sekta mbali mbali za kiuchumi na za kiutamaduni. Utendaji nao kwa namna moja ama nyingine unaathiriwa na sera za nchi katika sekta hizo. Wakati sera za kiuchumi uathiri shughuli za kiuchumi zinavyoendeshwa katika nchi, kitu gani kinazalisha na kutumiwa na nani, na ni nani anashikiria njia gani ya uchumi, sera za masuala ya jamii huiongoza jamii katika taratibu za maisha ya siku kwa siku. Kadhalika katika utawala ni sera za kiutawala zinazotoa mwongozo.&lt;br /&gt;Hatua ya kutunga na kurasmisha sera ni muhimu sana. Kutungwa kwa sera nako kunategemea nguvu za kisiasa ziko mikononi mwa nani na zinatumikaje. Aidha hatua ya kuamua nani awe na nguvu za kisiasa yaweza kutegemea sana itikadi iliyopo.&lt;br /&gt;Kwa mantiki hiyo, itikadi ya nchi au jumuiya fulani ndio kiini cha nguvu za kisiasa, cha sera, cha utendaji na cha mustakabali wa taifa.&lt;br /&gt;Hivyo, ni muhimu sana kuwa na itikadi iliyo njema ili mustakabali wa taifa uwe mwema pia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini itikadi ni sehemu tu ya siasa ya kundi husika. Katika ainisho, siasa ni njia za kutafuta na kupata nguvu, na vile vile ni njia anazozitumia/wanazozitumia mwenye/wenye nguvu katika kuhakikisha anabaki/wanabaki na nguvu hizo hususan za kiutawala ili afanye/ wafanye mazuri/mabaya kwa taifa/jamii kutegemeana na msukumo alionao/walionao. Kadhalika siasa ni kuamini kwamba njia fulani fulani zinawezesha ufikiaji wa malengo fulani. Lakini kama ulivyo msemo wa  kibusara, imani sharti iambatane na matendo, vinginevyo si imani kamili.&lt;br /&gt;Kwa mantiki hiyo siasa ina uwili/udaikotomi, yaani imani(itikadi) na mchakato wa utendaji.&lt;br /&gt;Kwa maneno mengine, kuna ngazi mbili zinazoweza kulipeleka taifa katika mustakabali mwema. Ngazi ya kwanza ni siasa katika itikadi, wakati ngazi ya pili ni siasa katika mchakato.&lt;br /&gt;Siasa katika mchakato, imegawanyika zaidi katika sehemu tatu, yaani maamuzi kwa kutegemea zilipo nguvu za kisiasa, utekelezaji utokanao na sera zilizopo za kiutawala, kiuchumi na kijamii. Hatimaye sehemu ya tatu ya mchakato ni matokeo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nayo sehemu ya maamuzi inategemea nguvu za kisiasa ziko mikononi mwa nani. Nguvu za fulani fulani za kisiasa zinaweza kuwa mikononi mwa mtu mmoja mmoja (individuals), au mikononi mwa wateule wa daraja fulani la juu katika jamii (elites) au katika vyama (parties) na au mikononi mwa watu(demos). Hapo ndipo panapoibuka dhana za aristokrasia, demokrasia, demokrasia ya vyama vingi, demokrasia huru, na dhana nyinginezo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Palipo na nguvu ndipo palipo na maamuzi na ndipo palipo na maelekezo ya kitu gani kitekelezwe kitu gani kiachwe. Maamuzi na maagizo ndizo sera. Hivyo chimbuko na aina ya sera ni nguvu ziko mikononi mwa nani.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kutoka nguvu ziliko tunapata sera za kiutawala. Ni sera hizi ambazo hutafsiriwa katika madaraka yaliyomo katika mihimili ya dola, hususan muundo wa serikali. Matharani, sera za kiutawala zaweza kuwa serikali kuundwa na chama kinachoshinda uchaguzi, serikali kuwa ya umoja wa kitaifa, madaraka serikali kuu (centralization), madaraka mikoani (decentralization)&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sera za kiuchumi huangilia masuala ya raslimali kuanzia mitaji fedha, nguvu kazi au suala zima la raslimaliwatu, na hadi rasilimali maliasili.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika sera kijamii kuna masuala ya utamaduni na huduma za jamii. Huduma za jamii ni pamoja na elimu, afya, ulinzi, usafiri na kadhalika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sera hizi katika mgawanyiko wake, zijapo pamoja katika kizitekeleza, ndizo huzalisha kiwango cha ustawi wa jamii husika, yaani mustakabali wa taifa/ jamii.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt; &lt;/div&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/6014809184859864743-8057906705033401966?l=georgekahangwa.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://georgekahangwa.blogspot.com/feeds/8057906705033401966/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=6014809184859864743&amp;postID=8057906705033401966' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/6014809184859864743/posts/default/8057906705033401966'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/6014809184859864743/posts/default/8057906705033401966'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://georgekahangwa.blogspot.com/2009/05/itikadi-na-mustakabari-wa-taifa.html' title='ITIKADI NA MUSTAKABARI WA TAIFA'/><author><name>Kahangwa</name><uri>http://www.blogger.com/profile/07414631690002879283</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='32' height='24' src='http://bp3.blogger.com/_3R2qky2qHsg/R9AwRuFfYjI/AAAAAAAAAAM/4OhJy7kgqsE/S220/george.jpg'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-6014809184859864743.post-9101796466565227634</id><published>2009-05-27T06:12:00.004-07:00</published><updated>2009-05-27T06:19:36.232-07:00</updated><title type='text'>ELIMU, MAARIFA NA UCHUMI</title><content type='html'>&lt;div align="justify"&gt;&lt;strong&gt;MAHOJIANO KATI YA HAPPY KATABAZI (MWANDISHI TANZANIA DAIMA) NA GEORGE KAHANGWA&lt;/strong&gt;&lt;/div&gt;&lt;div align="justify"&gt;&lt;strong&gt;Ni jinsi gani elimu inaweza kulisaidia taifa letu kiuchumi na kijamii katika ulimwengu wa sasa?&lt;br /&gt;&lt;/strong&gt;&lt;br /&gt;Takribani nyakati zote katika historia ya mwanadamu, elimu imekuwa ya manufaa sana kwa mtu mmoja mmoja anayeipata na kwa jamii ambayo mpata elimu anaishi. Leo hii zinapoendelea jitihada za kihimizana katika ngazi ya familia na taifa kwamba hapana budi kuwekeza sana katika suala la elimu bila suluhu, kimsingi sababu kuu ni hilo kwamba elimu ina manufaa kwa mtu binafsi (private returns) na kwa jamii (social returns). Ni dhahiri basi kwamba anapoelimika mtanzania mmoja ananufaika yeye na linanufaika taifa zima la Tanzania.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika ulimwengu wa sasa unaouzungumzia, manufaa hayo ya elimu yanazidi kutambulika na kuongezeka kiasi kwamba  katika mataifa mbali mbali hususan ya ulimwengu wa kwanza elimu inatazamwa kuwa ndilo tumaini la kipekee kiuchumi na kimaendeleo kwa sasa na kwa siku nyingi za usoni.&lt;br /&gt;Utakumbuka kwamba uchumi wa  nchi moja moja una msingi wake, matharani hapa Tanzania kwa miongo kadhaa tunazungumza kwamba kilimo ni uti wa mgongo wa taifa,kwa maneno mengine msingi mkuu wa uchumi wetu ni kilimo. Utakuwa unafahamu pia kwamba mataifa kadhaaa yaliyoendelea kiviwanda yanazungumzia uzalishaji wa viwandani kuwa ndio msingi mkuu wao kiuchumi (industrial economy)&lt;br /&gt;Mtazamo wa kidunia sasa hivi ni kwamba uchumi wa ulimwengu hususan wa mataifa yanayoitwa yaliyoendelea unahama katika kutegemea zaidi viwanda na sekta nyinginezo za uzalishaji, tegemeo kubwa sasa ni maarifa ambayo chimbuko lake ni elimu. Kwa kifupi tunaweza kusema kuwa dunia ya leo na kesho inaelekea zaidi katika uchumi wa maarifa (knowledge economy)&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nchi za ulimwengu wa tatu, ikiwemo Tanzania yetu zimedumu katika kutegemea kilimo, zikashindwa kuingia katika uchumi wa viwanda. Kwa sasa nchi hizi zinayo fursa ya kujikwamua na kutoka katika maendeleo duni  endapo zitajielekeza katika kuutafuta uchumi wa maarifa. Kwa mantiki hiyo nchi yetu inayo fura ya kuingia katika ulimwengu wa kwanza, bila kulazimika kutafuta ufalme wa viwanda mama, yatosha tukiuendea sasa kwa udi na uvumba uchumi wa maarifa. Elimu ndio chombo pekee cha kutupeleka huko.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni nini hasa unachokimaanisha kwa kusema uchumi wa maarifa na una uhakika gani kwamba kwa kuutafuta uchumi huo taifa letu litaondoka katika ulimwengu wa tatu?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ndugu mwandishi, upo ushahidi usiotiliwa shaka kutoka katika mataifa mbali mbali ambayo awali hayakufanikiwa sana katika uchumi wa viwanda yakaja kupata maendeleo makubwa sana kutokana na maarifa. Tuchukulie kwa mfano nchi ya Finland, kwa miongo kadhaa taifa hilo lilikuwa halina mafanikio makubwa kiuchumi, wafinn walitegemea sana zao la mbao na mara kwa mara uchumi wao uliyumba. Lakini tokea serikali ya nchi hiyo ilipofunguka macho ikawekeza kwa nguvu katika maarifa, filand kwa sasa limekuwa taifa lenye mafanikio makubwa sana kiuchumi kwa kiasi kilichoushangaza ulimwengu. Kwa sasa finland ni moja ya nchi chache sana duniani zinzoweza kutoa kwa raia wake elimu bure kuanzia elimu ya msingi hadi vyuo vikuu. Mataifa yaliyoko katika umoja wa nchi za ulaya yanaendelea kujifunza kwa bidii kile ambacho finland imekifanya, wakijua fika kuwa katika ulimwengu wa utandawazi ni maarifa pekee yatakaloliwezesha taifa kuwa na nguvu kubwa kiuchumi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa ufupi uchumi wa maarifa ni uchumi unaotegemea maarifa kama raslimali kuu. Unajua maliasili kama madini na ardhi ni rasilimali, fedha ni rasilimali hali kadhalika watu ni raslimali. Hizo ni raslimali zinazoshikika na kuonekana wazi (tangible resources) lakini maarifa ni tofauti kidogo maana ni intangible. Viel vile wakati rasilimali tangible hutumika na kuisha, rasilimali ya maarifa haiwezi kuisha bali huwa bora zaidi na kuongezeka kadiri inavyotumika.&lt;br /&gt;Uchumi huu wa maarifa unaeleweka zaidi unapochanganuliwa katika zile zinazoitwa nguzo zake kuu nne. Hizo nguzo ni Elimu na uendelezi wa rasilimali watu; pili, Utafiti, uvumbuzi na ubunifu; tatu, Tekinolojia na mawasiliano; na nne ,ni Mfumo wa utawala na nyenzo sahihi.&lt;br /&gt;Katika nguzo ya elimu na uendelezi wa rasilimali watu, ili taifa liufikie uchumi wa maarifa linatakiwa kuhakikisha kuwa elimu inayotolewa ina ubora wa hali ya juu na watu wa nchi husika wanaendelezwa kwa wingi, kama sio wote ili wafikie viwango vikubwa vya elimu na kuyapata maarifa watakayoyatumia kuujenga uchumi wao. Taifa halina budi kuhakikisha si tu kwamba halina raia yoyote mjinga bali pia asilimia kubwa ya raia ni wahitimu wa vyuo vikuu katika fani mbali mbali na ni wasiokoma kutafuta maarifa hata wawapo kazini na katika maisha yao yote ili wazidi kupata ujuzi wa kazi, wawe wazalishaji zaidi na washindani.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika nguzo ya utafiti, uvumbuzi na ubunifu taifa linatakiwa kuwa na mchakato endelevu wa kufanya tafiti zinazolenga kugundua maarifa mapya, suluhu za matatizo mbalimbali, ugunduzi wa nyenzo na uboreshaji wa zana za kazi. Tafiti za namna hiyo zitalifanya taifa kuboresha kila sekta ya uzalishaji na zaidi sana zitalinufaisha taifa kwa njia ya kuuza maarifa yaliyogunduliwa kwa mataifa mengine. Nadhani unafahamu ni kiasi gani wagunduzi wa vitu mbali mbali wanazinufaisha nchi zao kwa kile wanachokigundua. Chukulia mfano wa ugunduzi wa simu za mkononi unavyozinufaisha nchi zinazozalisha simu hizo. Ni wazi kuwa elimu yetu inapaswa kuwa na mkono katika hili, tunatakiwa kuwa na elimu inayomfanya mwanafunzi awe na uwezo wa kutafiti na kugundua maarifa mapya au kuwa mbunifu hata akaboresha yale yaliyopo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuhusu nguzo yya teknolojia na mawasiliano, taifa linapaswa kuwa la watu wenye kupata kwa wingi habari sahihi na zenye manufaa, wawe na mawasiliano ya kutosha tena ya haraka na wawe watumiaji wazuri wa teknolojia ya habari na mawasiliano kiasi kwamba njia hizo zinawasaidia kuzalisha mali zaidi,  na kwa wakati muafaka. Fikiria kwa mfano, unapokuwa na mkulima au mfanya biashara  anayeweza kupata mtandao unaomwezesha kupata habari za soko la mazao yake au bidhaa zake kutoka ulimwengu mzima, ni dhahiri mtu huyu akitumia habari hizo vizuri kamwe hatakuwa sawa na yule anayejua tu habari za soko la kijijini kwake. Hata katika hili elimu ina jukumu muhimu kwani ni kupitia katika elimu watu hujifunza matumizi ya teknolojia ya habari na mawasiliano.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nguzo ya nne ya mfumo wa utawala na nyenzo sahihi. Katika hili taifa linahitaji kuwa na mfumo unaowezesha maarifa yanayopatikana yanatumika vilivyo katika sekta za uzalishaji. Ili kufanikisha hilo hapana budi kuwe na uhusiano wa maana kati ya taasisi za elimu na sekta mbali mbali za uzalishaji. Matharani, kuwepo kwa uhusiano wa vyuo vikuu na sehemu za ajira ili kinachofunzwa vyuoni kiwe ni chenye manufaa mahali pa uzalishaji. Vile vile kuwe na mfumo unaowezesha maarifa kuzalishwa na kutumika katika nchi. Mfumo huo uwezeshe mambo kadhaa kama vile upatikanaji wa nyenzo za kufanyia tafiti, uhuru wa kujiendeleza kimaarifa mahali pa kazi na uhuru wa watu kufanya ugunduzi majaribio na ubunifu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;strong&gt;Unafikiri nguzo hizo za uchumi wa maarifa ziko katika hali gani hapa nchini, taifa letu linawezesha hayo unayoyasema?&lt;br /&gt;&lt;/strong&gt;&lt;br /&gt;Nchi yetu Tanzania, kwa kweli ina hali mbaya sana katika nguzo zote nne. Laiti kama tungekuwa vizuri katika japo nguzo mbili, uchumi wetu ungekuwa na hali nzuri kiasi chake. Elimu yetu imeendelea kuyumbisha na kuwa na hali duni kuanzia kile tunachokiamini na kukitekeleza kama falsafa ya elimu nchini, sera za elimu, mitaala, mchakato wa kufundisha na kujifunza, uwezeshaji wa watendaji katika elimu na suala zima la utadhimini wa elimu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukiangalia katika takwimu zilizotolewa hivi karibuni na benki ya dunia, Tanzania ina alama 7 kwa mia katika elimu na uendelezaji wa rasilimali watu, asilimia 17 katika utafiti na ugunduzi, asilimia 8 katika teknolojia ya habari na mawasiliano, na asilimia 34 katika mfumo na nyenzo. Kwa hiyo uchumi wetu unaitegemea rasilimali ya maarifa kwa asilimia takribani 17 tu, wakati yapo mataifa yamekwisha kufikia asilimia 90 na zaidi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Unaweza kung’amua kwa takwimu hizo jinsi taifa letu lilivyo na elimu isiyokidhi. Vile vile licha ya kwamba watanzania sasa tunakadiriwa kuwa milioni 39 watu wetu wengi hawajaendelezwa kiasi cha kulinufaisha taifa kiuchumi, tunayo rasilimali watu ya kutosha lakina bahati mbaya iliyokosa maarifa. Mwalimu Nyerere aliwahi kutuambia kwamba, ili nchi iendelee inahitaji pamoja na vitu vingine, watu wake. Lakini watu bila maarifa ni hasara tupu.&lt;br /&gt;Kwa upande wa tafiti nako hatuko vizuri kwa sababu nyingi, kwanza matharani katika vyuo vikuu, utakuta tafiti zinafanyika ndio, lakini si kwa maslahi ya taifa bali kwa wafadhili wan je wanaotoa fedha kwa ajili ya tafiti hizo. Ninachosema hapa ni kwamba watafiti wachache tulionao badala ya kutumiwa na taifa wanatumiwa na mashirika ya nje kufanya tafiti ambazo hao wageni wana maslahi nazo, na watafiti wetu wanakubali maana wanataka pesa. Laiti kama Taifa letu, hususan serikali kuu, ingeona haja ya kuwekeza katika utafiti na kuwawezesha watafiti wetu kutumia umahili wao katika kutafuta maarifa mapya, na kutafiti suluhu za matatizo yetu yote sisi wenyewe.&lt;br /&gt;Kibaya zaidi hata tafiti chache zilizokwisha fanyika nchini, matokeo ya tafiti hizo ni nadra kusikia yakitumiwa vilivyo katika sekta za uzalishaji. Ripoti nyingi za tafiti zimeishia kujaa vumbi katika shelf za maktaba za vyuo vikuu bila kutumiwa.&lt;br /&gt;Ama kwa suala la teknolojia ya habari na mawasiliano, licha ya kwamba hatujamudu kuingiza jambo hili katika shule zetu za sekondari, wengi miongoni mwa vijana wanaojua kutumia intertnet na vitu kama simu za mkononi bahati mbaya hawazitumii katika kiwango kizuri cha kuwanufaisha. Kwa walio wengi internet ni kwa ajili ya kutumiana ujumbe wa kirafiki, kuangalia picha za pono, hali kadhalika simu ni kusalimiana tu. Wachache sana wanaotumia mawasiliano kujiendeleza kielimu, kutafuta maarifa na au kupata habari za masoko na biashara.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;strong&gt;Unafikiri ni nini kifanyike?&lt;br /&gt;&lt;/strong&gt;Yapo mengi ya kufanya, labda mimi nizungumze kupitia jicho la taaluma yangu. Hatuna budi kuwa na sera za elimu zitakazotuhakikishia kwamba kila mwenye uwezo wa kupata elimu ya juu anaipata bila vikwazo vya karo, nafasi kidogo na kadhalika. Tunatakiwa kuongeza fursa kwa gharama yoyote ile, huo ni uwekezaji utakaotuletea manufaa makubwa sana kiuchumi kama nilivyoeleza.&lt;br /&gt;Hatuna budi pia kuwa na mitaala inayomwezesha mwanafunzi kuwa wa manufaa kabisa katika ulimwengu wa kisasa. Tunahitaji wahitimu wanaoajirika, tuahitaji elimu ituzalishie wagunduzi na wabunifu mahiri, watafiti wachapa kazi na watu wanaodumu katika kuyatafuta maarifa kwa bidii katika maisha yao yote.&lt;br /&gt;Kadri tutakavyoendelea na sera za kukopesha watu wachache waingie vyuo vikuu ndivyo tutakavyolididmiza taifa. Kadri tutakavyoipuuza taaluma ya ualimu ndivyo tutakavyo dunisha elimu yenyewe na kubaki kuwa wasindikizaji katika ulimwengu wa utandawazi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;strong&gt;Hujazungumzia manufaa ya elimu kijamii, unasemaje hapo?&lt;br /&gt;&lt;/strong&gt;Nimetaja jambo la social returns, lakini kwa upande mwingine elimu inapaswa kuinufaisha jamii kwa kuzalisha wahitimu waadilifu.kwa sasa mitaala yetu haijakaza sana suala la maadili na shule nyingi hazionekani zikiwaadilidha watanzania. Yamkini ndio sababu tuanpata wingi wa watumishi na viongozi wala rushwa, wabadhilifu na mafidsadi.&lt;br /&gt;Laity kama mitaala yetu yote kuanzia elimu ya awali hadi vyuo ingesisitiza vya kutosha elimu ya maadili. Tunatakiwa kuwa waadilifu katika mahusiano, katika kazi, katika utunzaji wa mazingira, katika utumiaji wa rasilimali na katika mwenendo kwa ujumla. Elimu inalojukumu la kutuhakikishia hilo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;strong&gt;Nini historia yako kwa ufupi?&lt;br /&gt;&lt;/strong&gt;Mimi ni mzaliwa wa mkoa wa kagera. Umri wangu ni miaka 39 sasa. Nimesoma elimu ya msingi katika shule ya Omurushenye na baadaye Bilele ya mjini Bukoba. Nilipata elimu ya sekondari katika shule ya Sekondari Bukoba. Nilisomea ualimu katika chuo cha ualimu Korogwe. Kwa miaka kadhaa nilikuwa mwalimu wa elimu ya Msingi. Baada ya kujiendeleza na kupata shahada ya kwanza ya ualimu katika chuo kikuu cha Dar es salaam, nilifungisha kwa miaka miwili mara hii elimu ya sekondari. Nilifanikiwa pia kusoma shahada ya uzamili katika elimu, hapa hapa chuo kikuu cha Dar es salaam, na hatimaye kuajiriwa na chuo hiki katika kitivo cha elimu, ambapo kazi yangu ni unadhiri katika masuala ya utawala wa elimu, mipango na sera. Nimepata pia mafunzo ya elimu na Utandawazi katika chuo Kikuu cha Oulu nchini Finland. Nimeoa na tuna mtoto mmoja.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;strong&gt;Ni nini matarajio yako ya baadaye?&lt;br /&gt;&lt;/strong&gt;Kwa taaluma yangu, inanipasa kujiendeleza zaidi na zaidi katika kuyatafuta maarifa. Natarajia kuanza masomo ya shahada ya juu ya falsafa huko ughaibuni mwishoni mwa mwezi huu. Bila shaka ninalo jukumu la kuitumia elimu yangu katika utumishi kwa taifa langu. Ndoto yangu ni kupata fursa pana za kuwahudumia na kuwatumikia watanzania wengi zaidi kama sio wote kwa kadri Mungu atakavyonipa kibali.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt; &lt;/div&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/6014809184859864743-9101796466565227634?l=georgekahangwa.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://georgekahangwa.blogspot.com/feeds/9101796466565227634/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=6014809184859864743&amp;postID=9101796466565227634' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/6014809184859864743/posts/default/9101796466565227634'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/6014809184859864743/posts/default/9101796466565227634'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://georgekahangwa.blogspot.com/2009/05/elimu-maarifa-na-uchumi.html' title='ELIMU, MAARIFA NA UCHUMI'/><author><name>Kahangwa</name><uri>http://www.blogger.com/profile/07414631690002879283</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='32' height='24' src='http://bp3.blogger.com/_3R2qky2qHsg/R9AwRuFfYjI/AAAAAAAAAAM/4OhJy7kgqsE/S220/george.jpg'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-6014809184859864743.post-7886439773674069436</id><published>2008-03-10T10:42:00.000-07:00</published><updated>2008-03-10T10:47:29.647-07:00</updated><title type='text'>UCHAMBUZI WA SERA YA ELIMU YA TANZANIA</title><content type='html'>WITO WA MJADALA WA KITAIFA KUHUSU MFUMO WA ELIMU TANZANIA&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ifuatayo ni sehemu yaliyomo katika mada kuu iliyotumika kuzindua mjadala wa elimu kitaifa kama ilivyotolewa na Mwl. George Kahangwa, mkufunzi wa shirika la elimu ya sheria Tanzania (TANLET), katika maadhimisho ya Nyerere day Oktoba 2006, ukumbi wa Manispaa ya Kinondoni; Dar es Salaam&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Utangulizi&lt;br /&gt;Watanzania katika ujumla wetu tunayo masuala yetu ya ndani ambayo yamevurugika sana na kutukosesha maendeleo.  Nguvu zetu na ushirikiano wetu ndio pekee utakaotusaidia kuyaweka sawa na kutupeleka kule tunakotaka. Tokea miaka ya mwanzo ya Uhuru wa nchi yetu, Baba wa Taifa Mwl. Julius Nyerere alitutaka tushirikiane na tutumie nguvu za pamoja kupigana vita dhidi ya maadui wetu ujinga, maradhi na umaskini. Miaka 45 sasa, tukiwa katika vita hivyo hatujaweza kumshinda angalau adui mmoja kati ya hao watatu. Hapana shaka tuna udhaifu mkubwa sana katika mapambano yetu, na udhaifu upo hasahasa katika sekta ya Elimu nchini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama elimu yetu isingekuwa na matatizo mbona tungeushinda ujinga, kwa Elimu tukaushinda umaskini na maradhi; kwa Elimu tukafikia kiwango kizuri cha maendeleo kama tulivyoshuhudia katika nchi za wenzetu (mathalani Japan na nchi za Scandinavia) waliotumia raslimaliwatu vizuri, wakawekeza katika elimu na sasa wako mbali sana kimaendeleo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tumekosea sana katika elimu kuanzia nini tunachokiamini, na tunachokitekeleza kupitia sera zetu na mipango mbalimbali ya elimu. Tumeshindwa kuwathamini askari wa mstari wa mbele katika vita vyetu (Walimu). Tumeendelea kutenga kiasi kidogo sana cha fedha kwa ajili ya sekta hii. Tumechezea mitaala na kuiyumbishayumbisha kana kwamba taifa hili halina dira wala mwelekeo. Taifa limegeuzwa kichwa cha mwendawazimu kwa kufanyiwa majaribio ya mara kwa mara ya nadharia za sera na mipango ya elimu isiyo endelevu na sera zisizoendana na ukweli wa kiutafiti ambazo mara zote zimefanya ubora wa elimu uzidi kuporomoka. Kwa mtindo huo taifa linaangamia kwa kupelekwa hatua moja mbele kisha hatua mbili nyuma ilihali ulimwengu wa utandawazi unasonga mbele kwa kasi, hautungojei.&lt;br /&gt;Yatosha sasa tulivyozunguka mlima wa matatizo, turejee katika mstari sahihi. Tujitathmini sisi wenyewe, tutambue madhaifu yetu, tujirekebishe, tukubaliane njia sahihi za kutupeleka mahali sahihi tena kwa haraka. Hakika tunahitaji kwanza kujadiliana kwa pamoja, tuangalie pamoja na mambo mengine, lile ambalo wadau mbalimbali wa elimu wametoa wito tulifanye, yaani “Mjadala wa kitaifa kuhusu elimu” mjadala wetu uangalie ni nini tulipanga kufanya kama nchi, kitu gani kinatekelezwa katika sekta ya elimu na ni kipi kilicho bora zaidi ambacho tungepaswa kufanya. Kwa maana hiyo mjadala huu uwe sehemu ya kutathmini mipango na utekelezaji wake kisha uibue mapendekezo yatakayoliokoa taifa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ili tuweze kuijadili vizuri mfumo wa elimu yetu hatuna budi kuangalia kwanza sera ya elimu inatotumika hapa nchini. Tuanze kwa tutafakari  nini maana ya neno sera.&lt;br /&gt;Sera yaweza kuwa ni mpango wa yatakayotendwa katika sekta fulani au ni maelezo ya malengo na njia ya utendaji iliyochaguliwa kuyafikia malengo hayo. Sera huwekwa katika maandishi ili iwe ndio kiongozi cha maamuzi ya nini kifanyike.&lt;br /&gt; Sera zaweza kuainishwa kwa namna mbalimbali ikiwa ni pamoja na ngazi zake mbili. Katika ngazi ya kwanza sera hubainisha masuala muhimu ya sekta fulani na kufafanua nia ya kisiasa ya kurekebisha au kuboresha vipengele mbalimbali vya mfumo wa sekta fulani. (Substantive policies)&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika ngazi ya pili sera huweka wazi utaratibu au namna ya utekelezaji wa kilichobainishwa katika masuala muhimu: nani mtekelezaji; utekelezaji ufanyikaje; kipindi cha utekelezaji; na ni raslimali gani zitumike. (Procedural policies) Hivyo sera ya elimu iliyokamilika na inayotekelezeka lazima iwe na ngazi zote mbili yaani sera bainishi na sera namna. Haya ni mabawa mawili yanayotegemeana. Sera nyingi zimekua dhaifu na zisizotekelezeka kwa kukosa bawa la pili; sera namna.&lt;br /&gt;Aidha yapo mambo kadhaa yanayofanya sera ifanikiwe. Miongoni mwa mambo hayo ni ushirikishaji kamilifu wa wadau wote wa sekta husika kuanzia hatua za mwanzo za uandaaji wa sera yenyewe, utekelezaji wake na kuifanyia tathmini sera hiyo.&lt;br /&gt; Elimu (kama sekta) inao wadau ambao ni pamoja na serikali kuu na serikali za mitaa, wamiliki wa Taasisi za Elimu za umma na binafsi, wazazi, walimu, wataalam wa elimu, wanafunzi, asasi zisizo za kiserikali, vyama vya siasa, jumuiya ya wafadhili, na wananchi kwa ujumla.&lt;br /&gt;Hapana shaka mjadala kuhusu elimu utakuwa haujakamilika kama utapuuza kuwashirikisha kikamilifu wadau wote hao. Hakika sera iitwayo ya Taifa na mipango yoyote isiyozingatia ushirikishwaji wa kundi fulani la wadau, kwa vyovyote vile ina walakini.&lt;br /&gt;Sera ya elimu inayotumika nchini Tanzania kwa sasa ni Sera ya Elimu na mafunzo ya mwaka 1995.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;a name="_Toc152757242"&gt;Yanayojiri nchini katika sekta ya elimu&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;Katika kipindi cha takribani mwaka mmoja sasa tangu serikali ya awamu ya nne chini ya uongozi wa Mheshimiwa Rais Jakaya Mrisho Kikwete, Wizara dada zinazohusika na utoaji wa Elimu nchini; yaani Wizara ya Elimu na Mafunzo chini ya Mheshimiwa waziri Magreth Simwanza Sitta na Wizara ya Sayansi Teknolojia na Elimu ya juu inayoongozwa kwa sasa na Mheshimiwa Waziri Profesa Peter Msolla; zimetenda mambo kadhaa ambayo yamemgusa kila mtanzania anayejali maendeleo ya taifa letu. Yaliyotendwa ni pamoja na jinsi wizara ya Sayansi, Teknolojia na Elimu ya Juu ilivyolishughika suala la mikopo ya wanafunzi wa Tanzania wanaosoma stashahada na shahada mbalimbali katika vyuo vikuu vya umma na vya binafsi nchini na nje ya nchi. Awali karibu na uchaguzi mkuu wa mwaka jana (2005) Serikali iliutangazia umma wa Watanzania kwamba fedha za mikopo zipo nyingi sana ila wakopaji ni wachache. Lakini mwaka huu (2006) Waziri wa sasa katika wizara husika akaliambia Bunge mjini Dodoma kwamba sasa mikopo ingetolewa kwa wanafunzi wa vyuo vya umma tu. Hilo nalo likatenguliwa kwa uamuzi mwingine kwamba wanaostahili ni wavulana wa daraja la kwanza na wasichana wa daraja la kwanza na la pili la kidato cha sita. Kutokana na maamuzi  hayo,watanzania kadhaa wakashindwa kujiunga na elimu ya juu wakiwemo yatima na maskini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa kweli maamuzi hayo ya wizara kwa niaba ya serikali si tu yalipunguza fursa za watanzania kupata elimu bali yalienda kinyume na sera ya Taifa ya elimu na mafunzo. Wakati sera katika kipengele chake cha 8.6, inaeleza nia ya serikali kuongeza udahili katika elimu ya juu, matamko ya wizara yalisigina nia hii njema ya kuhakikisha watanzania wengi zaidi wanapata elimu ya juu kwa ajili ya kuiendeleza nchi yetu.&lt;br /&gt;Vilevile katika kipengele cha 3.3 cha sera hiyo, inaelezwa kuwa serikali itasaidia jamii zisizobahatika (yatima, maskini na wengine) ziweze kupata fursa nyingi za elimu. Maamuzi ya wizara yaliweka kando hilo na kuamua kutumia madaraja ya kufaulu hata kama kuna maskini na yatima anastahili kuingia chuo kikuu lakini hana hilo daraja. Ama kwa hakika kusaidia hawa wasio na uwezo ndilo lengo hasa la kuundwa kwa Bodi ya Mikopo na kuwepo kwa mikopo yenyewe.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Aidha wakati kipengele cha 3 cha sera ya elimu kinazingatia kanuni ya fursa sawa kwa wote, maamuzi ya serikali yalikuwa na chembe za ubaguzi wa kitabaka, kijinsia, kinasaba, kidini, kikanda na kimaumbile. (Ubaguzi huu umeongeza manunguniko miongoni mwa waliokwisha shiriki mikutano ya mjadala huu, hata baadhi ya watu wakadhani ndio ajenda kuu ya mjadala)&lt;br /&gt;Vigezo hivyo vya utoaji wa mikopo kwa daraja la kwanza na la pili vimewekwa kwa namna ambayo inaonesha wazi kuwa serikali imeingilia mamlaka ya Bodi ya Mikopo ya wanafunzi, kinyume cha sheria namba 9 ya mwaka 1994 iliyounda Bodi hiyo ya Mikopo.  Sheria  hiyo sehemu ya 17(d) na kanuni ya Bodi ya mikopo ya 2004 pia nayo inaeleza kuwa kipaumbele kitatolewa kwa yatima, wenye ulemavu,wanawake katika masomo ya sayansi au uandisi na teknolojia. Kwa kutozingatia vigezo hivyo, maamuzi ya serikali yalikuwa yanakinzana si tu na sera, bali hata sheria ya Bodi ya Mikopo na katiba ya Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania. Kwa ufupi suala la mikopo limetuonyesha kwamba, ubora wa sera na mipango si tu maandishi yake bali ni pamoja na uwezo wa watekelezaji kuielewa, kuizingatia na kuitekeleza kwa umakini.&lt;br /&gt;Utekelezaji unaoendelea sasa umewaumiza wanyonge na umeifanya elimu ya juu nchini iendelee kuwa ya wateule wachache (elite). Wachache hao kamwe peke yao hawataweza kutupeleka kwenye kiwango cha maendeleo tunachokitaka. Ili nchi yetu iweze angalau kufikia hatua ya awali ya maendeleo kitekinolojia sharti asilimia 25% ya wanaoingia elimu ya msingi nchini waweze kudahiliwa katika elimu ya juu. Tanzania hadi kufikia mwaka 2001 tulikuwa kwenye asilimia 0.37%, katika hali yetu mahututi kiasi hicho bado tunawanyima watu mikopo ya kusoma!&lt;br /&gt;Kwa utendaji huo wa kuliangamiza taifa, watendaji yamkini wana agenda ya siri ya kujenga kwa maksudi taifa lenye wasomi kichele na alaiki ya mambumbumbu wasio na uwezo wa kushiriki masuala ya uchumi na siasa za nchi yao; wasioweza kuhoji utendaji wa viongozi wao na kuwawajibisha, wasioweza kukataa kuporwa kwa raslimali za nchi kwa njia ya mikataba inayonuka rushwa na ufisadi mwingine; wasioweza kushika nafasi za uongozi ili uongozi na utajiri ubaki mikononi mwa familia chache teule. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wizara ya elimu na mfunzo kwa upande wake imeishafanya mengi ikiwa ni pamoja na kuzingatia sera katika kipengele cha 6.2.5 kwa kurejesha masomo yaliyofutwa na waziri wa zamani, kipengele kinaweka wazi kuzingatiwa kwa masomo hayo katika mfumo mzima wa elimu. Kumbe tofauti ya mawaziri hawa  ni kiwango chao cha kutekeleza au kutotekeleza sera na mipango ipasavyo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Aidha wizara ya elimu katika kile kinachodaiwa ni kukabili upungufu wa walimu, imeamua kuwapeleka vijana waliomaliza kidato cha sita katika mafunzo ya mwezi mmoja ili wawe walimu wa sekondari na kuwaahidi shahada za chuo kikuu huria. Hatua hiyo ni kinyume na sera ya Elimu hususan kipengele chake namba 5.4.4 kinachoweka sharti kwamba, kiwango cha chini kabisa cha taaluma ya mwalimu wa sekondari iwe ya umma au ya binafsi kitakuwa Diploma ya Elimu tena iliyotolewa na chuo kinachotambulika. Kadhalika utendaji huo wa wizara unapingana na sera katika masuala ya ubora wa elimu na hitaji letu la kuwa na walimu mahiri, kama sera yenyewe inavyosema. Kibaya zaidi chuo kikuu uria cha Tanzania nacho kimenasa katika mtego usiokuwa wa kwake kwa kuandaa mpango huitwao ‘clash program’ wa kuwasomesha watanzania shahada ya ualimu kwa miaka miwili ilihali kinajua wapo walimu waliosoma shahada hiyo kwa miaka minne tena kwa kozi ya kuishi chuoni. Ni dhahiri hiyo haitakuwa shahada, kwa mujibu wa sera ni diploma.&lt;br /&gt;Mafunzo ya mwezi mmoja yameudhalilisha ualimu. Ualimu ni taaluma (Profession) haiwezi kufunzwa katika siku thelathini. Mwalimu ndiye mpiganaji wa mstari wa mbele katika vita yetu dhidi ya ujinga. Iwapo askari wa mgambo hawezi kufundishwa kwata tu akaambiwa nenda kasaidie angalau kikosi cha mstari wa akiba vitani kabla hajafunzwa shabaha, inakuwaje yanachukuliwa maamuzi ya namna hii katika taaluma nyeti ya ualimu na sekta ya elimu kwa ujumla. Ama kwa mfano mwingine, taifa letu lina uhaba wa madakitari hadi serikali inaamua kuwaita kazini waliostaafu, basi tuwapeleke vijana waliomaliza kidato cha sita wakasomee udakitari kwa mwezi mmoja. Kuna taaluma tatu zinazofanana kwa jinsi zinavyogusa moja kwa moja nafsi ya mtu; ukasisi unaoshughulika na roho; udaktari unaushughulikia mwili na ualimu unaoshughulikia akili. Zote tatu hazipaswi kuchezewa hata kidogo, hafundishwi Padri au Shehe kwa siku therathini. Mara nyingi mwalimu shuleni amefanya yote matatu.kumlea mtoto kiakili, kiroho na kimwili, iweje leo tumpe mtu mwenye wajibu mzito kiasi hicho mafunzo ya zimamoto. Labda tuwaulize hao waliosoma kwa siku 30, ninyi ni wataaluma ipi na mna cheti kipi kinachohalalisha huduma yenu? Jibu ni la wazi, ninyi sio walimu ondokeni mara moja mashuleni kama mnalipenda taifa letu, acheni kucheza na akili za watoto wa watanzania wasio na hatia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa nini serikali haijifunzi kutokana na makosa yaliyofanyika wakati wa utekelezaji wa mpango wa UPE miaka ya 1970 na 80. Alizolewa yeyote akapewa ualimu, madhara yake yanaliandama taifa hadi leo. Wakati umefika wa Tanzania kuwa taifa linalojifunza kutokana na wengine au makosa yetu wenyewe. Iweje hadi leo hatupendi kushugulikia mzizi wa tatizo tunakimbilia kuchukua maamuzi ya ilmradi.  Tunapuuza kabisa sababu zinazowafanya walimu wenye sifa waikimbie taaluma yao kila siku iendayo kwa Mungu. Matharani, siku kadhaa zilizopita iliripotiwa kutoka mkoani Mara kwamba walimu wa shule kadhaa za sekondari mkoani humo wamekimbia, kisa serikali tangia iwaajiri hawakuwahi kulipwa mishahara yao. Badala ya kushughulikia chanzo cha tatizo hili na kulitafutia ufumbuzi tunakurupuka kuajiri wasio na sifa za ualimu eti kujaza nafasi.&lt;br /&gt;Wakati tulionao si wa kuharibu zaidi. Ni wazi sasa kwamba ipo haja ya kujadili sera na mipango ya Elimu na mafunzo ili tukubaliane namna ya kudhibiti yanayotekelezwa katika sekta ya elimu yasiendelee kuliangamiza taifa.&lt;br /&gt; Mfumo wa elimu&lt;br /&gt;Watanzania tunatofautiana sana kifikira kuhusu mfumo wa elimu unaoifaa nchi yetu. Tofauti hizo zimejidhihirisha zaidi tangu kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi hapa nchini, ambapo kila chama kina mtizamo wake kuhusu elimu. Ikitokea vyama hivi vya siasa vikapishana mara kwa mara katika utawala wa nchi, na vyote hivi vina sera tofauti tofauti za elimu, balaa kubwa litaisibu sekta hii nyeti ya ELIMU.&lt;br /&gt;Tunavyo vyama vya siasa 18 vyenye usajili wa kudumu na takribani vitatu vyenye usajiri wa muda. Hivyo, zipo sera tofauti zaidi ya 18 kuhusu elimu. Je sera ya elimu ya taifa imejumuisha kwa kiasi gani michango kutoka sera za vyama vyote hivi ili kujenga mwafaka wa kitaifa kuhusu jambo hili nyeti? Ni wazi kuwa taifa linahitaji sera moja isiyoyumbayumba, inayokubalika kwa wadau wote wa elimu ili labda tofauti zetu zibaki katika mbinu za utekelezaji. Mjadala wa kitaifa ndio pekee waweza kutufikisha katika muafaka huo.&lt;br /&gt;Tuchukulie mfano wa kilichomo katika ilani za uchaguzi za vyama kwa ajili ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2005. Tutaona wazi kuwa elimu iko hatarini, kama hatutajadiliana, kuelewana na kukubaliana. Yapo maeneo ambayo ilani za vyama fulanifulani vinakubaliana na mengine vinatofautiana.maeneo hayo ni pamoja na Mfumo wa miaka ya elimu, Lugha ya kufundishia na namna ya Kugharimia elimu. Vyama kadhaa viliweka bayana katika ilani zake nia ya kuimarisha elimu ya awali katika maeneo yote nchini. Lakini kwenye suala la mfumo wa elimu, vyama vinatofautiana sana. Wakati vipo vyama vinayoshikiria mfumo wa miaka 2-7-4-2-3+, vingine vinaona bora miaka 2-8-4-2-3+, vingine miaka 2-11-1-3+&lt;br /&gt;Elimu ya msingi na suala la ajira&lt;br /&gt;Sera ya elimu inayotumika nchini inaeleza kuwa baada ya elimu ya msingi, mhitimu aweza kuingia katika ulimwengu wa kazi (kuajiriwa/kujiajiri). Tujiulize, elimu yetu ya msingi tuliyonayo sasa nchini na mitaala yake ilivyo, kweli yatosha kwa mtoto anapomaliza darasa la saba kuingia katika ajira, ajira ipi (ufanyakazi za ndani, uchangudoa, upigadebe na ‘unyoka’ katika machimbo ya madini, ukuli au umachinga?); na je ni ajira katika umri upi na si kinyume na sheria za kazi za shirika la kimataifa  (ILO) zinazozuia watoto wasiajiriwe/wasitumikishwe? Sera haielezi kama wahitimu wa elimu ya msingi wanao ujuzi wowote wa kuwawezesha kuingia katika soko huria lenye changamoto za utandawazi, sayansi na tekinolojia ya kisasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt; Mitaala ya elimu nchini&lt;br /&gt;Nchi yetu imekuwa na mabadiliko ya mara kwa mara ya mitaala karibu kila wizara ya elimu ilipopata uungozi mpya. Wizara ya Elimu imepata kuongozwa kwa vipindi tofauti na mawaziri ambao idadi yao sasa inafikia 16. Kila mmoja wa hawa aliingia madarakani na mikakati yake tofauti na wenzake. Tofauti hizo badala ya kuleta tija zimeikosesha sekta ya Elimu mwendelezo (continuity) na kuchangia uduni tunaouona leo katika elimu ya taifa. Kwa mfano ni wazi kuwa tofauti kati ya Waziri Jackson Makwetta na Waziri Joseph Mungai na sasa tofauti kati ya Mungai na Waziri Magreth Sitta imeyumbisha mno ubora wa mitaala ya elimu ya nchini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;a name="_Toc152757243"&gt;Bila mitaala mizuri na imara hakuna elimu bora. Laiti kila waziri angefuata msimamo wa sera ya kitaifa, elimu yetu isingekuwa duni kama tunayoijua leo. Kwa kuzingatia unyeti wa suala la mitaala, mnamo mwaka 1996 wadau wa elimu nchi waliwahi kuishauri serikali kutengeneza sera rasmi ya pekee kuhusu mitaala. Leo hii miaka kumi baadaye, watanzania hawajasikia lolote kuhusiana na kuzinduliwa kwa sera ya mitaala. Mjadala huu utusaidie ili serikali ilifanye hilo kwa maslahi ya taifa. Hakika tunahitaji mitaala isiyoyumbayumba tena iliyo sahihi.&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;a name="_Toc152757254"&gt; &lt;/a&gt;&lt;br /&gt;Bajeti na kugharimia elimu&lt;br /&gt;Watanzania hatuna budi kutafakari kwa kina mwelekeo wetu wa namna tunavyogharimia elimu kuanzia ya msingi hadi chuo kikuu. Jinsi elimu inavyogharimiwa kwa sasa ni mashaka matupu, ambapo bajeti ya serikali kwa ajili ya elimu imeedelea kuwa ndogo na matumaini ya watanzania maskini kupata elimu bora yanazidi kufifia. Matharani,suala la mikopo ya chuo kikuu linavyoshughulikiwa.&lt;br /&gt;Aidha tukirejea katika sera ya elimu nchini, miongoni mwa madhaifu ya sera hiyo ni kuwa na mambo yanayotofautiana au yanayopingana hususan kuhusu ni vipi tugharimie elimu na kwa maslahi ya nani. Mathalani wakati sera katika sura ya 3 inazungumzia upatikanaji wa elimu na fursa sawa (Access and equity) ikilenga kuwainua maskini, yatima na makundi mengine ya wasiobahatika, kwa upande mwingine inaweka upinzani kwa hilo katika sura ya 10 kipengele 10.2 inaposisitiza uchangiaji wa gharama za elimu bila kuonesha makundi ya wasioweza yataponea wapi.&lt;br /&gt;&lt;a name="_Toc152757246"&gt;. Tujiulize swali jingine katika mjadala huu, kwamba Wizara ya Elimu ilipofuta ada ya UPE iliweka njia gani mbadala kwa ajili ya kupata fedha za kugharimia elimu ya msingi nchini?&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;Na je tulipofuta ada ya UPE, huku bado tunazitaka halmashauri (kwa mujibu wa sera kipengele cha 10.2.12) zianzishe kodi maalum ya elimu kwa ajili ya kupata fedha za kuendesha elimu ya msingi, huku sio kujikanganya? Ukweli ni kwamba halmashauri nchini hadi sasa hazina kodi hiyo zimebaki kuwa tegemezi kwa serikali kuu na kwa fedha ya wafadhili.&lt;br /&gt;Sera pia inataja nia ya serikali kuboresha mgawo wa bajeti yake ya kila mwaka kwa ajili ya sekta ya elimu (kipengele 10.2.11). Lakini katika utekelezaji, bajeti ya elimu inapanda na kushuka mwaka hadi mwaka. Mathalani, mwaka ilipoandikwa sera (95/96), Elimu ilipata asilimia 15.3% ya bajeti, ikashuka hadi asilimia 10.5% mwaka 97/98. Ikaja kupanda hadi 22.1% mwaka 2001/02 lakini ikaporomoka tena hadi 15.1% mwaka 2004/05 Kuyumbayumba huku hakuendani na sera hata kidogo na kunaonesha jinsi ambavyo serikali imeshindwa kuweka kipaumbele na msimamo katika elimu. Wapo wadau wa elimu wanaopendekeza asilimia ya bajeti kwa ajili ya elimu ifikie 30% na zaidi. Kwa sasa ugharimiaji wa elimu nchini unategemea sana misaada toka nchi wafadhili na mikopo ya Benki ya Dunia. Ni vema tunavyosaidiwa, lakini watanzania tunapaswa kutafuta namna tutakavyo ongeza fedha za kugharimia elimu tusitegemee misaada siku zote.&lt;br /&gt;Kwa upande wa vyama vya siasa nchini, navyo vinatofautiana sanaa kuhusu namna ya kugharimia elimu. Matharani, wakati chama fulani msimamo wake ni serikali kutoa elimu ya bure kuanzia shule ya msingi hadi chuo kikuu, kingine kinasema mwanafunzi  atachangia elimu, kwa kufuata mpango wa kadri mwanafunzi atakavyofaulu vizuri zaidi ndivyo atakavyozidi kulipia gharama kidogo zaidi kwa ajili ya elimu&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Suala ubinafsishaji katika elimu&lt;br /&gt;Hivi karibuni nchi yetu iliingia katika ubinafsishaji ambao uliikumba pia sekta ya elimu. Hivi leo watu binafsi wanamiliki na kuendesha shule za awali, msingi, sekondari na vyuo Sera ya elimu itumikayo nchini inaunga mkono ubinafsishaji huu katika vipengele vingine mbalimbali,lakini Katika sura ya 3 sera hiyo hiyo inasisitiza dhana ya usawa katika kuwapatia watu wote elimu bora. Swali la kujiuliza ni, kwa kiasi gani tofauti za kitabaka zimeongezwa na kasi ya ongezeko la shule binafsi za gharama ya juu zenye mvuto wa kimaslahi na mazingira bora ya kazi kwa walimu, ilihali shule za umma hazina walimu. Ni dhahiri katika hili ubinafsishaji unamaanisha kutoweka kwa matumaini ya wanyonge. Naam, asiye na hela akaandikishe watoto wake katika shule zisizo na walimu, mtoto apate daraja la chini akose mkopo wa elimu ya juu, umaskini uzidi kushamiri katika familia yake. Yule mwenye pesa akasomeshe wanawe kwenye shule zenye walimu wa kutosha na wa akiba ili azidi kufaulu na kuneemeka.&lt;br /&gt;Tulipoamua kubinafsisha elimu, tungeona mbali ili kuepusha kupanuka kwa wigo wa matabaka katika jamii. Leo hii mshahara wa mwalimu mwenye shahada anayeanza kazi serikalini ni wastani wa sh. 230,000/=, wakati katika baadhi ya shule binafsi mwalimu mwenye sifa kama hizo ana mshahara mara mbili ya huo, ingawa naye mazingira yake ya kazi hayajawa mazuri. Serikali katika hali hiyo ya tofauti kubwa kimaslahi, isitegemee shule za umma zitakuwa na walimu bora. Lakini kwa kuwa Serikali inao uwezo kuliko wamiliki wa shule binafsi, muda umefika imheshimu mwalimu na kumboreshea maslahi yake. Ubinafsishaji ulipaswa kuzingatia haki ya kila mtoto wa kitanzania kufundishwa na mwalimu bora.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Matatizo ya walimu&lt;br /&gt;Suala la matatizo ya walimu nchini limekuwa wimbo wa muda mrefu bila ufumbuzi wake. Hatupaswi kuendelea na wimbo huu tena. Sharti ufumbuzi upatikane sasa.&lt;br /&gt;Sera ya elimu katika ukurasa wa 31 inaorodhesha matatizo hayo ya walimu, ikiwa ni pamoja na mishahara midogo, uhaba wa nyumba za walimu, hadhi ya chini ya taaluma ya ualimu na ukosefu wa nafasi za walimu kujiendeleza. Hatua zinazopendekezwa ndani ya sera kwa ajili ya kuondoa matatizo hayo ni za kiujumla sana. Kushindwa kwa sera kubainisha mikakati mahususi ya kuondoa kero zinazowakabili waalimu kumechangia kwa kiasi kikubwa usugu wa kero hizo ambazo zinaendelea kuwepo hadi leo. Ingefaa matatizo yanayawapata walimu wetu, yatafutiwe ufumbuzi wa kudumu haraka sana. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Aidha kuhusu taaluma yenyewe, kipengele cha 5.3.6 kinasisitiza kwamba taaluma ya chini ya mwalimu wa shule ya msingi itakuwa ni cheti cha ualimu daraja la kwanza. Kipengele kinakwepa kusema hali hiyo itakuwa imefikiwa ifikapo lini. Hivi leo miaka kumi na moja baada ya kuzinduliwa kwa sera hiyo, katika mikoa kadhaa, kwa mfano mkoa wa Lindi asilimia 44.3% bado ni walimu wa daraja B/C.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa upande wa ujuzi wa walimu wanaofundisha mashuleni, Taifa mwaka huu lina jumla ya walimu 47,536 ambao taaluma yao ni chini ya daraja A, wataendelezwa lini hawa? Inaelekea jitihada zinafanyika Dar es Salaam ambako asilimia 13.1% tu ndio wa daraja la B/C. Wakati huo huo tunaimba wimbo wa haki ya watanzania wote kupata maisha bora bila kuwa na shule bora, walimu wenye taaluma ya kutosha na kwa usawa. Dar es Salaam ina walimu 238 wenye shahada ya chuo kikuu walioko elimu ya msingi, wakati kwenye hiyohiyo, Lindi, Kagera, Mtwara, Mwanza, na Singida hawana hata mmoja!  Huu si umakini hata kidogo katika matumizi ya raslimali watu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt; Sera ya elimu inatambua kwamba mwalimu wa daraja la A ni yule aliyehitimu kidato cha nne na kupata mafunzo ya miaka miwili katika chuo cha ualimu, leo tunao waliopata mafunzo hayo kwa mwaka mmoja, hawa nao ni wa daraja gani?&lt;br /&gt; Wakati sera kwa kipengele namba 5.4.4 inasema kwamba kiwango cha chini cha taaluma ya mwalimu wa sekondari kitakuwa Diploma (bila kutaja ifikapo lini) Shule za sekondari za serikali mwaka huu (2006) zina walimu 1860 ambao ama hawana taaluma ya ualimu au wana cheti daraja la B/C; wapo pia walimu 196 wa cheti daraja A tu wanaofundisha katika shule za sekondari nchini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sera katika ukurasa wa 41 inazitupia lawama shule binafsi kwa kuendekeza ajira kwa walimu wasio na sifa (lakini hao wanaofundishwa kwa siku 30 wanaenda shule za serikali). Ukweli ni kwamba walimu wengi wenye shahada na walio mahiri wako katika shule za binafsi kwa sababu zinathamini ubinadamu wao na taaluma yao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sera katika ukurasa wa 46 inataja hitaji la haraka la kufundishwa walimu wengi zaidi, lakini leo hii idadi ya walimu tarajari wa cheti daraja A wanaojiunga na vyuo vya ualimu nchini inazidi kupungua, wakufunzi vyuoni wanapungua, vyuo vya ualimu vimepungua na fungu la bajeti ya serikali kwa ajili ya vyuo vya ualimu imeporomoka kutoka asilimia 2.6% mwaka 1997/98 hadi 1.1% mwaka huu 2006/07.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakufunzi wa vyuo vya ualimu kwa mujibu wa sera wanatakiwa wawe na elimu si chini ya shahada inayotambulika ya chuo kikuu (kipengele 5.5.5). Takwimu za mwaka huu zinaonesha kati ya wakufunzi 799 wa vyuo vya ualimu vya serikali ni 286 tu ndio wana shahada. Inakuwa ni jambo linaloshangaza sana, kwamba vyuo vya serikali vina wakufunzi 24 ambao hawana hata cheti cha daraja A (hao wanamfundisha nani, nini) wakati huo kuna walimu zaidi ya 200 wenye shahada ya chuo kikuu wako shule za msingi. Huo ni ushahidi mwingine wa matumizi mabaya ya rasilimali watu yanayoendekezwa na wizara husika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;a name="_Toc152757250"&gt;Lugha ya kufundishia&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;Eneo jingine tunalopaswa kujadili na kukubaliana ni suala la lugha ya kufundishia. Kwa muda mrefu sasa hapa nchini kumekuwa na mabishano ya lugha gani itumike kufundishia mashuleni..Japo tafiti mbalimbali zimethibitisha kwamba Kiswahili kingeweza kuboresha elimu yetu ya sekondari hadi vyuo, bado tumeendelea kung’ang’ania lugha ya mkoloni. Seraya elimu (ukurasa wa 52) inataja sababu za Tanzania kuendelea kutumia lugha ya kiingereza kama lugha ya kufundishia katika shule za sekondari.   Sababu hizo ni kuwawezesha watanzania kupata (to access) ujuzi na maarifa, sayansi na teknolojia na kuwasiliana na mataifa mengine. Tujiulize katika mjadala huu iwapo hayo hayawezi kupatikana kwa Kiswahili chetu na hivyo tuendelee kung’ang’ania kiingereza ambacho wapo wanaopata shida katika kufundisha au kujifunza kwa kiingereza. Hatuna mfano wa nchi yoyote katika ulimwengu wa kwanza iliyopata maendeleo ya Sayansi na Teknolojia kwa kutumia lugha ya kigeni.&lt;br /&gt;Aidha kipengele namba 5.5.8 cha sera kunasema kwamba lugha ya Kiswahili itakuwa somo la lazima kwa wanaosomea ualimu daraja A, diploma na shahada, Hili ni jambo jema lakini haliendani na ukweli kwamba katika vyuo vyetu vikuu wanafunzi wa shahada ya ualimu hawana kozi ya Kiswahili kama somo la lazima isipokuwa wale tu wanaochagua wenyewe kusoma Kiswahili. &lt;br /&gt; Kwa upande wa siasa, vipo vyama vya siasa nchini ambavyo vikiingia madarakani (si ajabu 2010) lugha ya kufundishia kuanzia chekechea hadi chuo kikuu itakuwa Kiswahili tu. Lakini vipo pia vyama ambavyo vikiingia madarakani vitataka lugha ya kufundishia iwe kiingereza tu. Ni wazi kuwa tusipojenga mwafaka wa taifa kuhusu masuala nyeti kama haya, ipo siku taifa litaingia katika matatizo makubwa. Mjadala huu utusaidie tupate suluhu ya suala hili pia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;a name="_Toc152757251"&gt;&lt;/a&gt;&lt;a name="_Toc152757252"&gt;Mitihani na malengo yake&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;Tunaitaji pia kuafikiana juu ya usahihi wa malengo ya mitiani itolewayo katika mfumo wetu wa elimu. Mingi imeonekana ikilenga kuchuja na kutupa waliowengi nje kusikojulikana na mingi inapima tu uwezo wa wanafunzi kukariri na kukumbuka kiasi kwamba nyanja nyingine za maarifa hususan ujuzi na stadi zimepuuzwa.&lt;br /&gt;Matharani, katika ukurasa wa 58 wa sera kuna maelezo kwamba mtihani wa darasa la IV lengo lake ni kupima uwezo wa wanafunzi katika kusoma, kuandika na kuhesabu (K3) na kuamua wandelee darasa la V au wakariri (warudie) darasa la IV. Ni heri tungepima K3 katika kiwango cha chekechea na sio darasa la juu kiasi hiki (la IV). Upungufu  mwingine ni kwamba, sera haitaji mwanafunzi aruhusiwe kurudia mara ngapi darasa la nne na baada ya hapo iweje?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mzazi mmoja ambaye mwanae alijikuta akirudia darasa la nne mara ya pili, alimfuata mwalimu mkuu shuleni na kumwambia hivi;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;“Mwalimu, unarudisharudisha tu mtoto bila kufikiria mimi mzazi nabeba mzigo gani? Sasa mimi nahesabu mwanangu yuko darasa la sita na mwakani anamaliza, miaka itayoongezeka hapo sare na madaftari utanunua wewe.”&lt;br /&gt;&lt;a name="_Toc152757249"&gt; &lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;a name="_Toc152757253"&gt;Nafasi ya tafiti na tathmini katika elimu&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;Sera nzuri za elimu au za sekta iwayo yoyote hazina budi kutungwa kutokana na ugunduzi wa tafiti za kina na hatimaye kutathminiwa mara kwa mara. Kipengele cha 6.4 cha sera ya Elimu na mafunzo kinazungumzia utafiti katika elimu na tathmini ya sera. Kipengele hiki kinazitupia lawama tafiti zinazofanyika nchini, kwamba hazina mwelekeo wa kusaidia kuunda sera na hazina mtazamo wa kiutendaji. Kipengele kinaendelea kulalama kwamba, watendaji katika vitengo husika vya tafiti wanaondoka na waliobaki wana utaalamu finyu katika masuala ya tafiti za elimu.  Ni dhahiri katika hali hiyo sera zinazotungwa nchini zimetungwa kisiasa zaidi na zinatekelezwa kisiasa kwa lengo la kutafuta umaarufu wa gharama ndogo miongoni mwa wapiga kura badala ya kujali ukweli uliothibitishwa kisayansi (ki-utafiti).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuna ukweli kwamba sera za elimu Tanzania hazina uhusiano na yale ambayo watafiti wameyathibitisha kupitia tafiti mbalimbali.  Mfano ni sera ya kuifanya elimu ya msingi kuwa bure (kufutwa kwa ada ya UPE).  Uamuzi huo ulipingana na tafiti zilizoonesha kwamba baadhi ya wazazi wa kitanzania (wengi) walikuwa na uwezo wa kulipa ada hiyo na wala ada ya UPE haikuwa miongoni mwa sababu kuu za watoto wa kitanzania kutoandikishwa au kutoendelea na shule. Sababu kuu za wazazi wa kitanzania kutowapeleka shule watoto wao ni pamoja na mchango wa watoto hao katika pato la familia kupitia kazi wanazotumikishwa kinyume cha sheria wasipoenda shule. Sababu nyingine ni utamaduni uliojengeka miongoni mwa jamii kadhaa za kitanzania kwamba mtoto wa kike hana haja ya kusoma shule .&lt;br /&gt;&lt;br /&gt; Aidha inashangaza kuona kwamba wanasiasa wanaohubiri kujitegemea na kuchangia gharama za huduma za jamii wanachukua uamuzi wa kufuta kabisa mchango huo wa wazazi na kuwatangazia watanzania kwamba elimu ya msingi ni bure (japo elimu toka enzi ya mkoloni haijawahi kuwa bure). Wakati huo huo wanalibebesha taifa mzigo wa deni la dola za kimarekani milioni 150 (sawa na fedha za kitanzania bilioni 202,na milioni500) kutoka Benki ya Dunia kwa ajili mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM). Yamkini, si vibaya kukopa kwa ajili ya maendeleo. Lakini Wataalam wa masuala ya sera, wanaonya kuwa, ili sera ifanikiwe, pamoja na mambo mengine isiwe na shinikizo au mkono mkubwa wa kutoka nje ya nchi.&lt;br /&gt;Mjadala huu utusaiidie kujiuliza, hivi Benki ya Dunia imetupatia mkopo huo ili tujitegemee au tuzidi kuwa tegemezi. Kama mkopo huu, tutaulipa kwa kodi zetu, tunashindwaje leo kutumia kodi hizo hizo maalum kugharamia elimu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt; Kwa ujumla, Sera za elimu nchini petu zimeghubikwa na tatizo la kukosa uhusiano kati ya ufafanuzi wa sera kisiasa na utekelezaji wa sera hizo. Kumekuwa na maelezo ya kinadharia na ya kialinacha ambayo hayatekelezeki. Mathalani Falsafa ya elimu ya kujitegemea ilitafsiriwa na kuekelezwa visivyo kisera na kisha Watanzania wakabakia kutupiana lawama kwa kutokuwa makini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Viongozi wetu wamekuwa na tabia ya kuibua sera mpya na kuanza kuzitekeleza bila utafiti wa kutosha. Matokeo ya tabia hii yamekuwa ni kufuta sera hii leo kisha kuirejesha kesho bila tahadhari wala maelezo ya kuridhisha. Sera ya Elimu na mafunzo ya mwaka 1995 inaonekana ‘kula matapishi’ maana imerejea kanuni ya zamani ya wazazi kulipa karo na kuruhusu watu binafsi kuendesha shule.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Huduma za Maktaba&lt;br /&gt;Sera katika kipengele cha 6.5 inataja matatizo ya Bodi ya Huduma za Maktaba nchini. Matatizo hayo ni pamoja na ukosefu wa vitabu vinavyoendana na wakati, uhaba wa wakhutubi wenye ujuzi, maktaba kukosa mawasiliano na taasisi mbalimbali, na watanzania kutokuwa na utamaduni wa kujisomea. Katika kipengele 6.5.1 badala ya sera kutaja ufumbuzi wa matatizo hayo inashikilia tu msimamo kwamba Bodi ya Maktaba itaendelea na huduma zake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;a name="_Toc152757256"&gt;Elimu maalum kwa wenye vipaji&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;Ama kuhusu suala la watoto wenye vipaji linalotajwa na sera katika kipengele namba 3.2.15, utekelazaji wake ni dhaifu mno kwani hadi sasa kigezo pekee kinachotumiwa kuamua mtoto mwenye kipaji ni alama alizopata kwenye mtihani wa mwisho. Kimsingi kuwa mwenye kipaji ni pamoja kudhihirisha uwezo usio wa kawaida kiakili, katika ubunifu, uongozi wa wengine, usanii na kipaji cha michezo.Je, wote wenye vipaji hivi Tanzania tumewatambua na kuwaweka katika shule maalum?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Aidha shule wanazopelekwa watoto hao hazina chochote cha umaalum cha kuvilea vipaji ipasavyo. Ni afadhali tu wangesoma katika shule za kawaida ili kuheshimu kanuni ya kusoma pamoja (inclusion) na kujiepusha na kiini macho cha shule maalum. Shule maalum za wenye vipaji zinaweza zisiwe muafaka kwa Tanzania kutokana na hali yetu kijamii, kiuchumi na kiutamaduni.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama kweli tuko makini na suala hili, sera isingetaja tu kwamba kutakuwa na chombo cha kuwatambua na kuwaendeleza watoto wenye vipaji, bali ingezitaka shule zote nchini kuwa na utaratibu wa kitaalam wa kuwatambua. Kwa jinsi hii, kila shule ingelazimika kutumia vigezo vya kitaaluma vya utambuzi wa vipaji.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt; Falsafa ya elimu ya kujitegemea&lt;br /&gt;Sera ya elimu pamoja na mambo mengine, imegusia falsafa ya elimu ya kujitegemea na suala la maadili katika elimu (values). Yafaa pia katika mjadala huu tutafakari mambo hayo pia. Sera inaitaja falsafa hii katika utangulizi, ukurasa wa ii na ix sera inapozungumzia Elimu na Maendeleo na inataja wazi kuwa elimu ya kujitegemea itaendelea kuwa ndio falsafa yetu ya elimu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tunafahamu kwamba elimu ya kujitegemea ni falsafa ilivyoasisiwa na marehemu Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere, miaka ya mwanzoni ya uhuru wa taifa letu. Falsafa hii iliweza kuendana na malengo ya elimu ya wakati wa kujenga ujamaa na kujitegemea hapa nchini. Kulingana na wakati tulio nao, mengi katika falsafa hiyo yanaonekana kusukumwa kando kwa sababu hasa za uchumi wa dunia ya leo, na si watanzania wote leo hii wanaamini bado katika ujamaa. Hivyo, tunahitaji ama kuiboresha falsafa hii au ipatikane falsafa mbadala kabisa ambayo inaweza kuendana vema na zama hizi za utandawazi, soko huria, ushindani na hata siasa za vyama vingi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Falsafa ya elimu ya kujitegemea ililenga kutatua matatizo yaliyosababishwa na elimu ya kikoloni. Ililenga pia kujenga jamii ya kitanzania na wasomi wanaoweza kulitumikia taifa hili kulingana na mazingira yetu ya ndani ya miaka ya mwanzo ya kujitawala. Wahitimu wa elimu walitarajiwa wapende kazi za mikono hususan katika sekta ya kilimo, ambayo inadaiwa kuwa ndio uti wa mgongo wa taifa.&lt;br /&gt;Changamoto tuliyonayo sasa ni kwamba, kama tuliweza kuondoa mapungufu katika elimu ya mkoloni, tusione aibu kuondoa mapungufu ya elimu ya kujitegemea labda kama hatuyaoni. Vile vile tujiulize tena, kwa sasa tunataka kujenga jamii ya namna gani. Elimu ya kujitegemea ni mtoto wa itikadi ya ujamaa na kujitegemea. Kadri muda unavyokwenda ndivyo wahubiri wa itikadi hiyo hapa nchini wanavyoiweka kando, hivyo wanayaweka kando pia malengo ya elimu ya kujitegemea.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tujiulize kama matumizi ya jembe au zana za kale za uzalishaji wa mahitaji ya binadamu tuliyonoyo hadi leo yalikuwa ndio tafsiri sahihi cha falsafa yenyewe ya kujitegemea hasa ilipozungumzia suala la watanzania kupenda kazi za mikono. Tujiulize sasa kama taifa lisilo na tekinolojia, uwezo wala mwelekeo wa kuzalisha mahitaji yake lenyewe litafikia malengo ya dira ya 2025. Ni dhahiri tunahitaji tekinolojia ya kisasa katika uzalishaji wa kila sekta na ni dhahiri pia kuwa uchumi za taifa utaimarika tu pale tutakapojijengea uwezo wetu wenyewe wa kuzalisha mahitaji yetu badala ya kutegemea kuagiza mahitaji hayo nchi za nje.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ingawa EK ilikuwa na malengo mazuri haionekani kama ilifanikiwa. EK ilitakiwa iboreshe uchumi wa vijijini na iwatayarishe wasomi kwa ajili ya maisha ya kijijini. Lakini leo hii miaka 39 tokea EK ianzishwe, vijiji vingi Tanzania vimebakia kuwa mahali pasipofaa kukaa si kwa wasomi wa elimu ya juu tu bali hata wahitimu wa elimu ya msingi wanazidi kupakimbia na kugeuka ‘wamachinga’ mijini. EK imeshindwa kuinua maisha ya vijijini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt; Kwa ujumla malengo ya EK yalipangwa vizuri sana kinadharia, lakini ilivyokuja kwenye utendaji wahusika ni kama vile hawakujua wafanye nini. Kwa wengi EK ilimaanisha tu kuwa na miradi ya bustani shuleni, mifugo na duka la shule hata kama wanafunzi hawajifunzi chochote kutokana na miradi hiyo. Ndio maana leo hii tusishangae miradi hiyo uongozi wa shule kadhaa nchini umeamua kuiendesha kwa mtindo wa ubinafsishaji.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Aidha EK hapa nchini imekumbwa na jeraha jingine la mauti tokea kuanzishwa kwa shule binafsi za msingi, sekondari na vyuo. EK iliweza kuzungumzika vizuri wakati serikali inahodhi umiliki wa shule, ni jinsi gani utamshawishi mmiliki wa English Medium Academy (ambako ni kimbilio la wenye uwezo wa kifedha) kwamba EK ifundishwe kwa jembe la mkono bustanini na si kompyuta kwenye mahabara.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati umefika ambao hatuna budi kuwa na falsafa ya elimu ambayo inalenga kuwafanya wahitimu wetu wa shule wawe raia wanaomudu kuzikabili changamoto za ulimwengu wa sasa. Enzi hizi, tunapozungumzia na kuingia katika ushirikiano wa kiuchumi na nchi mbalimbali, ambamo nguvu kazi imekuwa huru kuhama toka nchi moja hadi nyingine.wahitimu wetu sharti wawe wameandaliwa kumudu ushindani huo katika soko la kimataifa la ajira ili wasije kufanywa vibarua ndani ya nchi yao, na wengine waweze kwenda nchi jirani na kukubalika kwa uwezo wao. Mathalani watanzania tunahitaji kufanana na wenzetu wa Kenya na Uganda katika utaalamu na stadi tunazozimudu, tunapoelekea kwenye shirikisho la Afrika Mashariki.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ikumbukwe kwamba, falsafa ya elimu ndio inatakiwa iwe chimbuko la nini kiwe katika mitaala ya elimu na mafunzo. Falsafa hiyo pia ndio hutumika kutathmini na kukosoa malengo ya elimu Hivyo iwapo kilichomo katika mitaala yetu hakiendeni na falsafa tunayoiamini basi mitaala hiyo ni potofu. Na kama mitaala inaendana na mahitaji ya wakati wa sasa na wa baadaye ila inatofautiana na falsafa, hatuwezi kusema tuko makini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Maadili katika Elimu&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kipengele 2.3.2 cha sera kinataja haja ya elimu kuinua maadili na utamaduni wetu. Tatizo la maadili katika elimu lina uhusiano wa karibu na tatizo la falsafa. Kwa jinsi itikadi ya ujamaa ilivyoamua falsafa ya elimu, ndivyo itikadi hiyo ilivyoelekeza yapi yawe maadili ya elimu. Wakati wa uongozi wa Baba wa Taifa, maadili ya elimu yalikuwa ya kijamaa, ndio maana watoto walikariri mashuleni pamoja na mambo mengine kwamba ujamaa na kujitegemea ndio njia ya pekee ya kujenga jamii ya watu walio sawa na huru. Aidha watoto walikariri ahadi za mwana TANU, sijui kwa nini watoto hao ukubwani walio wengi wamesaliti yote hayo. Leo hii ujamaa tunao tu kwenye Katiba ya Jamuhuri ya muungano lakini hata Baba wa Taifa alifariki akijua umekwisha toweshwa nchini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tatizo la maadili linajitokeza ifuatavyo;&lt;br /&gt;Kwamba chini ya mfumo wa vyama vingi vya siasa ambako karibu kila wafuasi wa chama fulani wana itikadi yao, ni dhahiri haieleweki ni maadili gani ambayo tumeyaweka wazi katika mitaala ili yaendane na mfumo wa kisiasa uliopo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwamba japo kinachoendelea katika uchumi wetu ni cha itikadi za kiliberali bado sera ya elimu haioneshi au iko kimya iwapo maadili ya kiliberali yanapaswa kuwemo katika mitaala au la. Kuna tofauti kubwa kati ya hali halisi kiuchumi na maadili yafundishwayo mashuleni hivi leo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwamba walimu wetu, wako katika mkanganyiko wa ama wafundishe ujamaa na maadili yake au wajiunge na upepo wa sasa wawafundishe watoto mitizamo ya kiliberali. Mjadala utusaidie tujue moja.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tuzingatie kwamba uliberali umeyafungulia milango maadili ya kigeni (kizungu) kuingia nchini kwa kasi (mengine mazuri mengine mabaya) na kuwa maadili hayo yamewateka vijana wetu na jamii kwa ujumla. Maadili hayo tunaona yakiambatana na utumiaji wa madawa ya kulevya, ushoga, uzuraraji, kuzungumzia mambo ya kujamiiana hadharani hata mbele ya watoto, itikadi kali na mmomonyoko wa maadili kwa ujumla.  Hivyo sera haitaji/haibainishi njia sahihi za kutumika nchini kwa ajili ya kufundisha maadili mema na utamaduni wetu mashuleni, tunaishia kuiga tu wanachofanya wenzetu ambao jamii zao zimeharibika zaidi kimaadili bila kujiuliza wanakosea wapi  (wapo wanaoamini kwamba mmomonyoko wa maadili ni kwa sababu kadhaa ikiwemo kuwatesa walimu wetu kimaslahi na kupiga marufuku viboko mashuleni)&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Eneo jingine linaloifanya sera hii istahili kujadiliwa au kutathminiwa, ni kusheheni kwake takwimu na taarifa za zamani ambazo nyingine zimepitwa na wakati. Ni jambo muafaka kwamba sera hii iandikwe upya (revised edition) na mjadala huu utupeleke hapo.&lt;br /&gt; MAPENDEKEZO&lt;br /&gt; Kwa kuwa matatizo ya elimu nchini ni lukuki, majadiliano yetu yaangalie si yale tu yatajwayo katika mada hii bali elimu kwa ujumla wake, ili hatima ya mjadala iwe kuibuliwa kwa sera ya elimu na mafunzo yenye ubora wa kipekee, tunayoikubali wote tena inayotekelezeka.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt; Tutumie fursa ya mjadala huu kuwataka watekelezaji katika sekta ya Elimu wazingatie dira yetu inayobainishwa katika sera zilizo rasmi na iwe mwiko kuchukua maamuzi yanayoliondoa taifa katika mwelekeo unaokubalika na ulio sahihi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Vile vile tuzingatie katika kujadili kwetu kwamba ni kazi bure kuongelea elimu bora bila mitaala bora tena inayozingatia wakati tulionao na ujao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt; Mjadala huu pia, utupeleke mahali ambapo tunaweza kusema kumdhalilisha mwalimu na taaluma ya ualimu sasa basi. Mathalani, tuwe na sheria inayouhesabu ucheleweshaji wa mishahara na maslahi mengine ya walimu kwamba ni udhalilishaji, ni kunyume cha haki za binadamu na ni kosa la jinai (kumtesa mtu). Pia tuwe na utaratibu unaompa heshima ya pekee mwalimu. Kama tunadiriki kuwaambia walimu kila mara kwamba kazi yao ni ya wito, basi tusione taabu kuwapa heshima ileile ya kijamii wanayopewa watumishi wengine wa wito, matharani viongozi na watumishi wa dini.&lt;br /&gt;Kuhusu suala la ukosefu wa nyumba za walimu, iwe marufuku kufungua shule mpya ambayo haina nyumba za walimu, nyumba zenye hadhi tena kwa idadi inayoendana na ikama itakiwayo. Aidha iwe haki ya mwalimu kupewa nyumba ya kuishi na mwajiri (entitled) Na mwalimu asipelekwe katika shule fulani bila mwajiri kumhakikishia nyumba ya kuishi na familia yake.&lt;br /&gt; Katika kumwendeleza mwalimu kitaaluma, uwe wajibu wa mwajiri (serikali au binafsi) ndani ya mkataba wa kazi kumwendeleza mwalimu kila baada ya muda uliotajwa wazi, kupitia njia ya mafunzo kazini na nyinginezo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuhusiana na tatizo linalojitokeza la matumizi mabaya ya raslimali watu, mjadala wa kitaifa utusaidie tuwapange walimu wetu (askari wetu dhidi ya ujinga) katika mstari wanapostahili kuwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Vile vile tujadiliane tupate ufumbuzi ambao ungefaa kwa matatizo ya makitaba na wananchi kutopenda kujisomea. Suluhu yaweza kuwa ni pamoja na kuwafundisha walimu hata wa shule za msingi ukhutubi ili waboreshe huduma za maktaba kwa wanafunzi mashuleni. Hili liendane pamoja na kuzitaka mamlaka husika kuhakikisha kila shule ina maktaba.&lt;br /&gt;Aidha ingefaa maktaba za umma ziwe wazi siku na saa ambazo watu hawako katika shughuli za kujipatia riziki, maktaba zitafaa sana kama zitakuwa kama sehemu ya watu kuburudisha akili zao baada ya uchovu wa kazi yaani ziwe na vivutio vya burudani, na ziwe wazi siku za mapumziko na watanzania wafahamishwe hilo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt; Falsafa ya elimu tunayoihitaji sasa ni ile itakayomwezesha mtanzania kuwaza kama raia wa ulimwengu mzima wakati huohuo akiweza kutenda kazi kulingana na mazingira ya nyumbani.  Falsafa ya elimu imwezeshayo mtu kumudu maisha wakati wote mahali popote katika uso wa dunia yetu&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ingefaa tuwe na sera ya elimu inayotaja bayana maadili ya kufundishwa kupitia elimu. Na isiishie tu kuyataja bali itaje na njia za kuyafundisha. Wataalamu wanataja njia tano za ufundishaji maadili ambazo tunaweza kuziingiza katika sera yetu na kuwafundisha walimu wetu kuzitumia (inculcation-kufunda, moral development-kukuza mwenendo, analysis-kuchambua, value clarification-kufafanua maadili na action learning-mafunzo vitendo)&lt;br /&gt;Kwa maoni yangu, kupitia masomo ya uraia, michezo, muziki na sanaa mbalimbali akili za watoto wetu tuzijengee maadili ya kidemokrasia, uaminifu kwa matendo, mawazo na maneno, uzalendo, uwajibikaji, utawala bora wa mali binafsi na za umma, uchapakazi, utunzaji mazingira, kujiamini, kujisimamia, kusaidiana, heshima, kujali, haki, usawa,uvumilivu,ustaarabu na mengine. Wanafunzi wafundwe maadili haya si katika nadharia tu kama ilivyozoeleka bali waingizwe katika vitendo halisi na waone mfano bora kutoka kwa viongozi na jamii yote inayowazunguka.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Inatubidi tambue umuhimu wa kupanua elimu ya lazima kwa kila mtanzania iwe si chini ya kidato cha nne ili kulipatia taifa watu wenye ujuzi na uwezo kushiriki barabara katika miradi ya kuondoa umaskini na maradhi na wenye uwezo wa kuhoji na kuwajibisha viongozi. Pasipo kupanua elimu ya lazima (ya msingi) tutajikuta hatuna uwezo wa kupanua elimu ya juu na hivyo hatutapata nguvu kazi ya kutosha yenye taaluma za kati na za juu kitekinolojia. Vivyo hivyo, ikiwa tunasita kuwekeza ipasavyo katika elimu ya juu kwa kuwapa mikopo wahitimu wote wenye sifa za kudahiliwa, maendeleo ya taifa letu yatabaki kuwa ndoto ya mchana. Hatuna budi kusahihisha makosa yote tuliyoyafanya katika sekta ya elimu, vinginevyo tusilie tukiona kuwa soko la ajira la Jumuiya ya Afrika Mashariki linatawaliwa na Wakenya, Waganda, Warundi na Wanyarwanda walioamua kuelewa nini maana ya kuwapa elimu bora raia wote, tusilalamike iwapo tutalazimika kuambulia kazi za kilalahoi tu katika shirikisho la Afrika Mashariki lijalo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Zaidi ya yote tutumie akili zetu na tafiti za wataalamu wetu kutafuta na kutumia ipasavyo vyanzo vyote vya fedha vinavyowezekana kwa ajili ya kugharimia elimu. Vinginevyo mipango yetu itaendelea kupendeza kwenye karatasi na elimu bora itabaki njozi. Miongoni mwa vyanzo vinavyoweza kufaa ni fungu kubwa zaidi kutoka bajeti ya serikali, kodi maalum ya elimu, ushuru maalum matharani katika vinywaji vikali, michango ya kila mwezi ya makampuni au mashirika yanayozalisha faida kubwa na kadhalika,&lt;br /&gt;&lt;br /&gt; &lt;a name="_Toc152757258"&gt;HITIMISHO&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;Wakati umekwisha wa kuendelea kuwa mashuhuda wa kudidimia kwa sekta ya elimu nchini bila kufanya jitihada za maksudi tena madhubuti sote kwa pamoja kuliokoa taifa letu Tanzania.&lt;br /&gt;Hatuna budi kutafuta haraka ufumbuzi wa matatizo yote ya elimu kama tunalitakia taifa letu mema. Tujadiliane kwa nia njema, tuitathmini sera yetu ya elimu kwa kina. Tuangalie wapi tunakosea, wapi tunafanikiwa, nini kinatukwamisha na nini tufanye. Hatimaye tuibuke na dira moja madhubuti itakayotuhakikishia kufika salama kwenye bandari ya maendeleo tunayoyatamani.&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/6014809184859864743-7886439773674069436?l=georgekahangwa.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://georgekahangwa.blogspot.com/feeds/7886439773674069436/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=6014809184859864743&amp;postID=7886439773674069436' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/6014809184859864743/posts/default/7886439773674069436'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/6014809184859864743/posts/default/7886439773674069436'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://georgekahangwa.blogspot.com/2008/03/uchambuzi-wa-sera-ya-elimu-ya-tanzania.html' title='UCHAMBUZI WA SERA YA ELIMU YA TANZANIA'/><author><name>Kahangwa</name><uri>http://www.blogger.com/profile/07414631690002879283</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='32' height='24' src='http://bp3.blogger.com/_3R2qky2qHsg/R9AwRuFfYjI/AAAAAAAAAAM/4OhJy7kgqsE/S220/george.jpg'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-6014809184859864743.post-9200120126399652056</id><published>2008-02-19T00:39:00.000-08:00</published><updated>2008-02-19T00:40:29.140-08:00</updated><title type='text'>HAKI HUINUA TAIFA</title><content type='html'>&lt;div align="justify"&gt; ITIKADI YA HAKI (JUSTICISM)&lt;br /&gt;&lt;br /&gt; YALIYOMO&lt;br /&gt;Utangulizi&lt;br /&gt;Falsafa ya Haki&lt;br /&gt;Dhana ya Haki&lt;br /&gt;Mafundisho ya kidini kuhusu haki&lt;br /&gt;Haki kama Itikadi&lt;br /&gt;Mfumo Haki wa Uchumi&lt;br /&gt;Mfumo Haki wa Kisiasa&lt;br /&gt;Mfumo Haki wa Kijamii&lt;br /&gt;Mfumo wa Sheria zitendazo Haki&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;SEHEMU YA KWANZA&lt;br /&gt;UTANGULIZI&lt;br /&gt;Historia nzima ya kuwepo kwa mwanadamu hapa duniani inathibitisha wajibu alionao mwanadamu wa kufanya shughuli mbalimbali ili kujipatia riziki na au kuyaendesha maisha yake. Shughuli hizo zinamlazimu mwanadamu kuwa na mahusiano mazuri na mazingira yanayomzunguka ili kutoka katika mazingira hayo apate anachokihitaji. Kadiri mazingira yanavyokuwa bora ndivyo maisha ya mwanadamu yanavyostawi vyema. Ila kwa kadri mazingira yanavyoharibiwa ndivyo maisha ya mwanadamu yanavyokuwa hatarini. Kwa ufupi maisha ya mwanadamu huyategemea mazingira karibu kwa kila kitu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Matharani, mwanadamu wa kale aliyeishi kwa kuwinda, kukusanya mizizi na matunda aliitegemea mimea na wanyama waliomo katika mazingira ili kupata mahitaji yake hayo. Alifika mahali uwindaji na ukusanyaji wake ukamtaka awe na zana za kufanyia shughuli hizo. Hata katika hili la kupata zana aliyategemea mazingira hayo hayo. Kutoka katika mazingira akaweza kupata mawe akatengeneza zana za mawe, kisha akagundua chuma na teknolojia yake, hatimaye akawa kiumbe anayeboresha zana zake kwa kugundua tekinolojia bora zaidi mara kwa mara.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwanadamu vilevile akawa kiumbe asiyeweza kufanya kazi peke yake bila kushirikiana na wanadamu wenzake. Wanadamu wa kale walishirikiana kuwinda na kukusanya kisha kugawana sawa kilichopatikana. Haki ilitendeka na ilipaswa kuendelea kutendeka. Kadri siku zilivyokwenda ukaibuka mgawanyo wa kazi ukichochewa zaidi na ugunduzi wa tekinolojia zilizoboresha zana za kazi pamoja na ugunduzi wa mambo mengine mbalimbali kama vile dawa za matibabu na kadhalika. Wale waliokuwa vinara wa ugunduzi fulani ukafika wakati wakawa wanatumia muda mwingi kuzalisha teknolojia yao na kutoa huduma kwa waliohitaji kutumia teknolojia yao, ilihali watu wengine waliendelea na shughuli za kawaida. Shughuli hizo za kawaida zilihitaji zana zilizotengenezwa na wale wachache wagunduzi. Hali imekuwa ndio hiyo hadi leo.&lt;br /&gt;Wakati huo huo kadri wanadamu walivyozaliana na kuongezeka, tabia mbali mbali tofauti zilijitokeza miongoni mwao. Pakajitokeza haja ya uongozi ili uweze kusimamia utaratibu unaokubalika na unaolinda maslahi ya kila mmoja. Lakini kwa hulka ya mwanadamu ubinafsi ukajitokeza, wengine wakawa na tabia ya kujipendelea kiasi cha kuwadhulumu wengine, baadhi ya waliopewa dhamana ya kuongoza wenzao wakatumia nafasi hizo vibaya kujinufaisha na kuwakandamiza wengine. Yakajitokeza mambo mengi yanayofanana na hayo, usawa ukatoweka madaraja na tofauti za watu zikajitokeza wengi wakapata zaidi ya haki yao, wengine wakakosa kilicho haki yao. Wakati huo huo mwanadamu akaendela kutumia kilichomo katika mazingira kwa kasi iliyohatarisha kutoweka kwa baadhi ya vitu vilivyomo katika mazingira hayo. Viumbe wengine wakawa hawana cha kuwatetea dhidi ya uhitaji wa mwanadamu unaoongezeka siku kwa siku.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Miongoni mwa wanadamu, wapo walioiona hatari ya hali hiyo ya kutotendeana haki tena miongoni mwa wanadamu wenyewe kwa wenyewe, na hatari ya matumizi ya mazingira yasiyo na utaratibu mzuri.  Wenye fikra hawa waliweza kujenga hata nadharia za mahusiano ya watu wenyewe kwa wenyewe na mazingira yao yakoje, yamepitia hatua gani na yanastahili kuwaje.  Wenye fikra wakaibua mawazo ya kwamba mahusiano haya yamepitia katika mifumo ya ujima, utumwa, ukabaila, ubepari na ujamaa. Wanabainisha zaidi kwamba kati ya mifumo hiyo mitano ni miwili tu ambayo ilionekana kuwa na kiwango kikubwa cha kujali maslahi ya kila mmoja, nayo ni ujima na ujamaa. Matharani katika ujima, watu waliwinda na kukusanya pamoja, mwisho wa siku wakagawana sawa haki ikatendaka. Lakini ulipojitokeza mfumo wa utumwa haki (ya mtumwa ikatoweka) mmiliki wa mtumwa akapata zaidi ya haki yake akawa yeye ndio binadamu na aliye mtumwa hadhi yake sawa na mnyama wa kazi. Katika mfumo wa ukabaila nako haki ilitoweka, ikawekwa tu mkononi mwa mwenye kumiliki ardhi. Hali kadhalika katika mfumo wa ubepari, mwenye haki akawa ni mmiliki wa mtaji na mfanya kazi haki yake ikanyongwa. Katika ujamaa kukajitokeza dhana ambayo ililenga kurejesha haki, kwamba umiliki wa mali uwe wa umma/ watu wote kwa pamoja. Lakini mfumo huu nao ukawa na madhaifu yake haki ya wote haikupatikana.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika miongo ya hivi karibuni, dunia ilishuhudia ushindani kati ya kambi mbili zinazoamini katika mifumo tofauti ubepari (uliokomaa ukawa ubeberu) kwa upande mmoja na ujamaa (ulioelekezwa kwenye ukomunist) kwa upande mwingine. Mifumo hii ikachukuliwa kuwa ndio imani (itikadi) za watu kisiasa, kiuchumi na kiutamaduni. Wengine huzitambua itikadi hizi kama mirengo, mmoja mrengo wa kulia na wa pili mrengo wa kushoto. Katikati ya mirengo hii miwili wakaibuka wenye kuchukia maovu ya ubepari lakini hawapendi mwelekeo wa kupita kiasi wa ujamaa. Wakaitwa hawa mrengo wa kati, miongoni mwao wakawa wale wanaoshikira itikadi ya Demokrasia ya Kijamii.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Miaka ya karibuni zaidi, imeshuhudua vile vile ubepari/ ubeberu ukishamiri na kuzizidi nguvu itikadi nyinginezo. Ukatanua makucha yake hasa baada ya kusambaratika kwa shirikisho la nchi za kisovieti za urusi (USSR) miaka ya 1990. Ubeberu umejitanua zaidi siku hizi kupitia dhana za utandawazi, soko huria na uwekezaji wa kimataifa. Haki ya waliowengi/ haki ya wote iliyotakiwa kuwepo tokea enzi za ujima haijapatikana. Laiti mifumo hii yote ingeamini katika kulinda haki ya kila mmoja bila suluhu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;SEHEMU YA PILI&lt;br /&gt;FALSAFA YA HAKI&lt;br /&gt;Kimsingi shughuli zote za mwanadamu na mahusiano ya watu hapa duniani yalipaswa kuwa ni kwa ajili ya kuboresha hali yake kimwili, kiakili, kiroho na  kuongeza ubora wa mahusiano yake na viumbe wengine. Hivyo, mchakato wa kila shughuli afanyayo ulipaswa kuwa katika namna ambayo haina dhuluma, uonevu, madhalilisho, taabu, ubaguzi, wala vikwazo kwa mwanadamu awaye yeyote na kwa kiumbe hai kingine chochote.&lt;br /&gt;Hali hiyo ya mchakato ulio mwema inawezekana pale tu mifumo iliyopo ya kisiasa, kiuchumi na kijamii imeelekezwa katika kiwango cha juu kabisa cha kuzingatia haki ya kila mtu. Dunia itakuwa mahali bora pa kuishi endapo tu kutakuwa na HAKI KILA SIKU, HAKI KILA MAHALI, HAKI KWA KILA MMOJA. Palipo na haki pana utunzaji na utumiaji mzuri sana wa mazingira, pana mahusiano mazuri ya kiwango cha juu cha ustarabu na pana amani, maana amani ni tunda la haki.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;SEHEMU YA TATU&lt;br /&gt;DHANA YA HAKI&lt;br /&gt;Zipo nadharia na maelezo mengi kuhusu dhana ya haki na umuhimu wake. Hapa nitatolea mfano wa mitazamo ya wanafalsafa japo wawili kuhusu haki.&lt;br /&gt;Mwanafalsafa aitwaye Aristotle (katika karne ya 4 K.K), alibainisha manufaa ya uwepo wa haki kwa watu aliposema maeneno yafuatayo.&lt;br /&gt;            ‘Kilele cha uwepo wa haki ni kuzalishwa na kutunzwa kwa furaha ya jamii na ya dola’&lt;br /&gt;Kwa maana hiyo, jamii kamwe haiwezi kuwa na furaha ya kweli kama haki haitawali na wala dola haliwezi kusimama imara pasina kutunzwa kwa kiwango kikubwa haki ndani ya mipaka ya dola husika.&lt;br /&gt;Aristotle alifafanua zaidi kwamba kwamba, kimsingi kuna aina mbili za haki ambazo ni kama ifuatavyo&lt;br /&gt;(i)                  Haki katika sheria&lt;br /&gt;(ii)                Haki katika gawio stahili&lt;br /&gt;Haki inapotambuliwa katika sheria kunakuwa hakuna upendeleo wala ubabaishaji (arbitrariness)&lt;br /&gt;Ili haki iwepo katika gawio, hapana budi kuwa na usawa. Watu sawa hupokea gawio sawa, watu wasio sawa hupokea gawio lisilo sawa. Usawa ni sehemu ya haki. Usawa unakuwepo pale tu ambapo hakuna anayejisikia kunyonywa au kunyimwa stahili yake (Jown Rawls, 1957). Watu huhisi kutendewa visivyo haki pale matarajio yao yasipotimilizwa au pale wenye mamlaka wanapowanyima stahili zao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kanuni za haki katika jamii huwezesha kufafanuliwa vema kwa haki na wajibu wa kila mtu na wa taasisi za jamii. Kanuni hizo pia, hueleza ni nani anayestahili kunufaika na raslimali na matunda ya kazi ya jamii husika.  &lt;br /&gt;Mwanafalsafa huyu wa masuala ya kisiasa &lt;a title="John Rawls" href="http://en.wikipedia.org/wiki/John_Rawls"&gt;John Rawls&lt;/a&gt; (1921-2002) alijenga hoja zake k akitohoa katika mtizamo wa kiutopia wa Bentham na Mill, mawazo ya mkataba wa kijamiii ya Locke na mawazo ya Kant kuhusu haki. Rawls  aliuelezea mtizamo wake wa kwanza na wa kimsingi kuhusu haki kama aliyoandika katika kitabu chake kiitwacho A Theory of Justice (1971) ambamo alipendekeza kwamba kila mtu anayo heshima ya kipekee  ambayo msingi wake ni haki ambayo hata haki za pamoja za jamii haziwezi kuizidi hiyo haki ya mtu mmoja mmoja.&lt;br /&gt;Kwa maana hiyo kanuni za haki zinakataa kwamba kumnyang’anya mtu uhuru wake kunahalalishwa na maslahi ya wengi. Mawazo ya Rawls yameainishwa tena katika kitabu kiitwacho Political Liberalism (1993),ambamo anaitazama jamii  kama "mfumo mwema wa ushirikiano miongoni mwa watu uliodumu kwa muda fulani kutoka kizazi kimoja hadi kingine. &lt;br /&gt;Jamii zote za wanadamu zina mfumo wa kimsingi wa kijamii, kiuchumi, na taasisi za kisiasa zilizo rasmi na zisizo rasmi. Katika kutibitisha ni jinsi gani vipengere hivyo vya mfumo hufanya kazi kwa pamoja, mtaalamu huyo Rawls alifanya jaribio kuhusu nadharia za uhalali wa mikataba ya kimfumo iliyomo katika kijamii. ili kutambua kama mfumo fulani unaoathiri mipangilio ya kijamii una uhalali, alisisitiza kwamba mtu hana budi kutazama kukubalika kwa mfumo huo miongoni mwa watu wanaoongozwa na mfumo husika. Yamkini si rahisi kumshirikisha kila mwana jamii katika kura ya maoni ili kubaini kiwango cha kukubalika kwa mfumo fulani miongoni mwa wanajamii, ila  kila mwana jamii ana uelewa na mara nyingi anafanya maamuzi ya busara kwa kiwango cha kulidhisha, yahusuyo mfumo wa jamii yake. Kwa kuzingatia hayo, Rawls alitengeneza hoja ya hatua mbili za kuzingatia katika mchakato wa kutabua kinadharia jinsi gani wanajamii wanaweza kuukubali mfumo  fulani :&lt;br /&gt;Hatua ya kwanza;&lt;br /&gt;Mwanajamii ukubali kuwakilishwa na mtu X kwa madhumuni fulani; kwa kiwango hicho, mtu X anakuwa amepewa mamlaka au nguvu, kama mdhamini wa haki za mwanajamii anayewakilishwa;&lt;br /&gt;Hatua ya pili;&lt;br /&gt;Mtu X hukubali kwamba matumizi ya kani fulani (sheria, kanuni, maagizo na amri) katika mtazamo wa kijamii ni halali kwa mujibu wa mamlaka aliyopewa. kwahiyo wanajamii wanabanwa na uamuzi wao wenyewe  wa kukubali wawakilishwe maadamu uwakilishi ni tendo la udhamini.&lt;br /&gt;Ukweli uliomo ndani ya hatua hizi, unakubalika kila panapotokea mtu mmoja anawakilisha kundi la watu liwe dogo au kubwa. ( matharani, mtu anapopewa dhamana ya kuratibu tafrija  ndogo anapoamua ni vazi gani litumike katika tafrija hiyo ni kwa sababu kakubalika na kupewa mamlaka ambayo sasa anayatumia kuamua kwa niaba ya wote)&lt;br /&gt;Hatua hizi vilevile, zinakubalika katika ngazi ya kitaifa ambapo serikali kama chombo kilichopewa dhamana kuu, hubeba nguvu za uwakilishi kwa manufaa ya raia wote walio ndani ya mipaka ya nchi husika. Endapo serikali itashindwa kutekeleza majukumu yake na kuhifadhi maslahi ya wananchi kwa mujibu wa kanuni za haki, serikali hiyo si halali maana inakuwa imevunja mkataba wa dhamana iliyopewa.&lt;br /&gt;Hata hivyo licha ya kwamba mwakilishi anakuwa amepewa mamlaka ya matumizi ya kani, kanuni kuu inayomwongoza inabaki kuwa kwamba, haki huchipuka au hutokana na watu na si shuruti toka kwa watunga sheria wenye mamlaka ya kiserikali. Ni lazima wenye mamlaka wazingatie uhuru walionao wanajamii. Rawls alidokeza pia kwamba, haki humpa mwanajamii uhuru kwa namna zifuatazo;&lt;br /&gt;Uhuru wa kifikra / uhuru wa kufikiri&lt;br /&gt;Uhuru wa utashi wa nafsi katika mahusiano ya mtu kijamii kwa mujibu wa imani yake ya kidini, falsafa na maadili yanayomwongoza mtu.&lt;br /&gt;uhuru wa kisiasa (mfano kuwepo kwa taasisi za demokrasia ya uwakilishi, uhuru wa kujieleza, wa vyombo vya habari na wa kukusanyika)&lt;br /&gt;uhuru wa kujumuika na kushirikiana na wanajamii&lt;br /&gt;uhuru wa mtu kwenda atakako na kuchagua kazi aitakayo bila kukinzana na misingi ya uadilifu&lt;br /&gt;uhuru wa kupata haki binafsi zinazolindwa na utawala wa sheria.&lt;br /&gt;SEHEMU YA NNE&lt;br /&gt;MAFUNDISHO YA KIDINI KUHUSU HAKI&lt;br /&gt;Dini nyingi zinapoeleza kuhusu uendeshaji wa nchi hapa duniani zinasema; HAKI HUINUA TAIFA.&lt;br /&gt; Mafundisho ya kikristo yanajumuisha suala zima la utu. Mojawapo ya mambo ya kipekee katika mafundisho hayo ni suala la kuwajali maskini zaidi katika jamii. Mawili kati ya maeneo saba ya mafunzo ya kikristo yanagusia suala la haki ya kijamii ni haya yafuatayo:&lt;br /&gt;Thamani ya maisha na utu wa mtu (Life and dignity of the human person): msingi wa mafundisho yote ya kikristo ni utakatifu wa maisha ya mtu na hadhi ya utu. Maisha ya mtu yana thamani kuliko chochote kile iwe umiliki wa mali au kitu kingine.&lt;br /&gt;Fursa kwa maskini na walioko katika mazingira magumu: Mhasisi wa imani ya kikiristo,Yesu Kristo mwenyewe alifundisha kwamba, siku ya kiama Mungu atamhoji kila mmoja wetu ni kitu gani alifanya kuwasaidia maskini na wahitaji: " Amini,nawaambia, lolote mlilowafanyia hawa ndugu zangu walio wadogo, mlinifanyia mimi”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kanisa huzidi kufundisha kwamba, kwa maneno, maombi na matendo mtu sharti aoneshe mshikamano na upendo wake kwa maskini.  Zinapotengenezwa sera za umma hapana budi fursa za maskini zipewe kipaumbele.&lt;br /&gt;Ama kwa hakika kipimo cha uadilifu wa jamii yoyote ile ni jinsi jamii husika inavyowachukulia wanajamii hiyo walio katika mazingira magumu.&lt;br /&gt;Hata kabla ya kusisistizwa katika rasmi mafundisho ya kikristo (hususan kanisa la kikatoliki), haki ya kijamii ilijitokeza sana katika masuala ya historia ya kanisa hilo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Matharani,&lt;br /&gt;Neno haki ya kijamii liliasisiwa na mkatoliki, Bwana Jesuit Luigi Taparelli mnamo miaka ya 1840, msingi wake ukiwa ni mafundisho ya Thomas Aquinas. Taparelli aliandika kwa mapana sana juu ya jambo hili katika jarida liitwalo Civiltà Cattolica, makala zake zilichambua nadharia za ubepari na ujamaa kama zinavyotazamwa katika mtazamo wa kikatoliki wa kanuni za asili. Msingi wa hoja zake ni kwamba nadharia hizi mbili za kiuchumi zinazohasimiana zinauhujumu umoja wa jamii. Si ubepari wa kiliberali wala ukomunisti ambao ulijali au ulijihusisha na falsafa ya maadili ya umma.&lt;br /&gt;Naye Papa Leo wa 13 ambaye alifunzwa chini ya Taparelli, aliandika andiko liitwalo Rerum Novarum mnamo mwaka 1891 (kuhusu hali ya tabaka la wafanyakazi). Katika andiko hilo, Papa aliukataa mifumo yote miwili ya kijamaa na kibepari, bali akautetea utaratibu wa kuwepo kwa vyama vya wafanyakazi na umiliki wa mali binafsi kwa mtu mmoja mmoja. Alifafanua kwamba, jamii haina budi kujengwa katika misingi ya ushirikiano na si kwenye migogoro baina ya madaraja ya watu, wala kwenye ushindani. Katika andiko hilo Papa Leo alitoa kauli ya kanisa Katoliki kuhusiana na na kuyumba kwa jamii wakati ule na migogoro ya kazi iliyoshamiri wakati wa mapinduzi ya viwanda, mitafaruku iliyopelekea kuibuka kwa ujamaa (the rise of socialism). Papa alisistiza kwamba wajibu wa dola ( serikali, mahakama na bunge) uwe ni kulinda na kukuza haki ya kijamii (na si vinginevyo), kanisa kwa upande wake lifanye kazi ya kuongelea masuala ya jamii kwa lengo la kufundisha misingi sahihi ya kiutu na maelewano katika jamii.&lt;br /&gt;Kwa upande wake Papa Pius wa 11 kwenye andiko liitwalo Quadragesimo Anno, la mwaka 1931 (kuhusu kuujenga upya  utaratibu wa jamii) yeye anafundisha kwamba haki ya kijamii ni suala la sifa ya utu wa mtu mmoja mmoja ( personal virtue), na kwamba jamii inaweza kuwa yenye haki pale tu mwanajamii hiyo mmoja mmoja ni mwenye haki. &lt;br /&gt;Papa wa sasa, Papa Benedict wa 16, katika andiko liitwalo Deus Caritas Est (Mungu ni pendo) anafundisha kwamba haki ya kijamii ndilo suala la kimsingi ambalo siasa zimepaswa kuhusika nalo, wakati suala kuu la kijamii linalolihusu kanisa ni usamaria mwema (usaidizi kwa wanajamii wahitaji)&lt;br /&gt;Aidha, msimamo rasmi wa kanisa katoliki kuhusu haki ya kijamii umeelezwa katika kitabu kiitwacho Compendium of the Social Doctrine of the Church, cha mwaka  2004 kilichohaririwa mwaka  2006.&lt;br /&gt;SEHEMU YA TANO&lt;br /&gt;HAKI KAMA ITIKADI&lt;br /&gt;Kwa kuwa haki ndio pekee iwezayo kumwakikishia kila mtu maisha mema binafsi na utengemano katika jamii, ni jambo jema jamii zikaiamini haki kama jambo la kipekee liwezalo kumwinua mwanadamu mmoja mmoja, jamii kwa ujumla na mataifa yote. Kwa maana hiyo ulimwengu unahitaji haki si tu kama itikadi ya kisiasa bali mwongozo wa kila mchakato wa shughuli za mwanadamu.&lt;br /&gt;Haki ndio itikadi mbadala ya usoshalisti, ubepari na michepuo yake ambazo ni itikadi zilizothibitika kuwa na mapungufu mengi na zimeshindwa kuwapatia watu wote kile wanachokihitaji. Tunahitaji kufikiri sasa, na kuona haja ya kuwa na itikadi ya haki ambayo hakika vizazi na vizazi vitaiamini na kuifuata kwa kuwa ndio pekee inayomhakikishia kila mtu mustakabari mwema.&lt;br /&gt;Itikadi katika ainisho rahisi ni imani kuhusu mahusiano kati ya watu na mfumo wa maisha katika jamii; kuna Itikadi zinazotetea mtu kumnyonya mwingine; pia zipo itikadi zinazokataa unyonyaji lakini hazidhibiti utegaji katika uwajibikaji na wakati mwingine hazina wepesi wa kutambua juhudi za mtu mmojammoja.&lt;br /&gt;Ni ukweli ulio bayana kwamba kitu ambacho mwanadamu mahali popote awapo anakihitaji ni HAKI.  Wanadamu kwa ujumla wetu, ili tuweze kuishi kwa mahusiano mema ya hali ya juu, kila mmoja wetu anapaswa kuamini katika HAKI yake mwenyewe, ya kila aitwaye mwanadamu na ya kila kiitwacho kiumbe hai.&lt;br /&gt;Hakika itikadi stahili na ya kipekee kabisa kwa ajili ya mstakabali mwema wa maisha duniani ni HAKI (JUSTICISM).&lt;br /&gt;Kutokana na itikadi hii, tutakuwa na mfumo haki wa uchumi (justifiable economy); mfumo haki wa kisiasa (justifiable political system); mfumo haki wa jamii (justice driven social system) na sheria zitendazo haki (just laws). Kwa maana hiyo, waamini wa itikadi ya HAKI, lolote lisilo haki si tu kwamba watalipinga bali watajiepusha nalo milele hata ukamilifu wa nyakati. Hakika itikadi hii itayainua mataifa, italiendeleza Taifa liwalo lolote.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Itikadi ya HAKI haiko mbali sana na yale ambayo baadhi ya wanamageuzi katika nchi mbalimbali duniani, kwa muda mrefu wamekuwa wakiyaamini kisiasa. Pengine ni suala la muda tu vyama vya siasa katika nchi mbali mbali vitaona haja ya kutamka rasmi na wazi kabisa kwamba itikadi yao ni HAKI.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;SEHEMU YA SITA&lt;br /&gt;MFUMO HAKI WA UCHUMI (JUSTIFIABLE ECONOMY)&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mfumo wa uchumi unaoheshimu haki unatambua uwepo wa haki ya raslimali asili, haki ya mwenye mtaji na haki ya mwenye nguvukazi. Mfumo huu unasisitiza kwamba sharti kuwepo maridhiasawa (amicability) kati ya pande tatu; raslimali asili, mtaji na nguvukazi au kati ya pande mbili; mtaji na nguvukazi/ raslimali asili na nguvukazi; kuhusu gawio (dividend) la uzalishaji. Maridhiasawa yanaweza kufahamika kimahesabu kwa kutambua thamani ya mtaji = (kizio chake ni HISA) na thamani ya nguvu kazi = ustadi wa nguvukazi x masaa ya kazi x 1% ya mtaji (kizio chake ni HISA-SHIRIKI)&lt;br /&gt;Itikadi ya haki inasisitiza kuwa, daima rasilimali za nchi fulani ni mali ya wananchi husika na kamwe haimilikishwi kwa watu wasiokuwa raia wa nchi hiyo. Chini ya itikadi hii sharti mwenye mtaji aumiliki kihalali na si vinginevyo. Vile vile mfumo haki hauruhusu mtu awaye yeyote kupata gawio lisitahililo nguvukazi kama mtu huyo hakuitumia nguvukazi yake katika uzalishaji husika. Aidha mwenye nguvukazi sharti aitumie kujipatia ridhiki na kuiendeleza jamii yake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;SEHEMU YA SABA&lt;br /&gt;MFUMO HAKI WA KISIASA (JUSTIFIABLE POLITICAL SYSTEM)&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mfumo wa siasa unaoheshimu haki unazingatia utashi na uamuzi wa kila mtu, unatambua haki ya mtu kuwa mfuasi wa chama cha siasa na hiyo unaruhusu uwepo wa mfumo wa vyama vingi vya siasa na demokrasia huru katika dola moja (Multi party system and free democracy) chini ya mfumo huu, itikadi ya mtu kisiasa au kutokuwa mfuasi wa itikadi yoyote haiwi sababu ya yeye kubughudhiwa katika nchi yake, kunyimwa ajira ya utumishi wa umma au kupewa dhamana ya uongozi wa umma uwe wa kuchaguliwa au kuteuliwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;SEHEMU YA NANE&lt;br /&gt;MFUMO HAKI WA KIJAMII (SOCIAL JUSTICE)&lt;br /&gt;Mfumo wa jamii unaoheshimu haki unazingatia usawa wa watu wote bila kutazama tofauti za rangi ya mtu, asili yake, jinsia yake, umri au daraja lake kimapato. Mahali ambapo mfumo haki umesitawi hkuwezi kujitokeza tena hali ya kukandamizwa kwa baadhi ya jamii za watu kama ilivyowahi kutokea na inavyoendelea kujitokeza katika historia ya dunia yetu. Dunia imeshuhudia kukandamizwa kwa haki ya jamii za watu weusi wenye asili ya Afrika popote ulimwenguni tangia enzi ya kuchukuliwa utumwani, ukoloni, ubaguzi wa rangi hadi kuibiwa kwa maliasili za mtu mweusi. Dunia pia ina rekodi ya kutengwa kwa wahindi wekundu huko bara la Amerika kulikofanywa na jamii za watu wasio wa asili ya bara hilo. Kadhalika mambo makubwa ya kuvunjwa kwa haki ya jamii yalifanywa dhidi ya watu asilia wa Australia waitwao waaboligini. Chini ya mfumo wa haki ya jamii, hayo yote hayatasikika tena, kamwe.&lt;br /&gt;Mfumo haki huifanya jamii iwe huru dhidi ya unyanyasaji wa kijinsia, udhalilishaji wa watoto na uonevu wa namna yoyote ile. Habari ya huyu ni mwanaume na huyu ni mwanamke na hiyo stahili yake si sawa na ya mwingine, hufikia ukomo chini ya mfumo haki. Mfumo huu unatambua kuwa mfumo wa kibaolojia kwa ajili ya kuendeleza kizazi cha viumbe katu si sababu ya kufanya kuwepo kwa utofauti baina ya jinsia mbele ya haki na wajibu. Chini ya mfumo huu jamii itawajali kwa kiwango cha juu sana wasiojiweza, wazee, yatima na wote ambao kwa sababu zilizoko nje ya uwezo wao hawawezi kujisaidia.&lt;br /&gt;Aidha mfumo huu huimiza ustarabu wa hali ya juu na huondoa kabisa tamaduni na mila zilizo kinyume na haki za binadamu. Ni mfumo unaoheshimu uhuru wa kuabudu, wa kujumuika na kushirikiana miongoni mwa wanajamii.&lt;br /&gt;Haki ya kijamii maana yake ni kuwa na jamii yenye taratibu za haki. Yaani kuwa na jamii ambayo inampa mtu mmoja mmoja na/au vikundi vya watu fursa na stahili sawa. Hakika kila mtu angependa kuishi katika jamii yenye haki ingawa mirengo tofauti huitazama haki kitofautitofauti. Dhana hii ya haki ya kijamii hutumiwa sana na mirengo inayoamini kwamba katika jamii zetu leo hakuna haki, matharani mrengo wa kushoto ambao unatetea kugawana sawa mapato na ushirika . mrengo wa kushoto katika mtazamo wake hutoa hoja kwamba haki ya kijamii kwa njia ya soko huria na hisani . kimsingi mirengo hii miwili hukubaliana juu ya umuhimu wa utawala wa sheria, haki za binadamu an welfare safety net.&lt;br /&gt;Haki ya kijamii wakati mwingine ina  mwonekano usio wa kisiasa bali wa kifalsafa zaidi. Haki ya kijamii imekuwa katika mafundisho ya kikatoliki na ni miongoni mwa misingi minne ya vyama vya kijani. Haki ya kijamii pia ni dhana inayotumiwa na wanaharakati wa ujenzi wa dunia yenye haki. Kwa wao haki ya kijamii misingi yake ni haki za binadamu na usawa.&lt;br /&gt;&lt;a name="Catholic_social_teaching"&gt;&lt;/a&gt;&lt;a name="The_Green_Party"&gt;&lt;/a&gt;Haki ya kijamii ni moja ya nguzo kuu za vyama vya kijani. Haki ya kijamii ambayo wakati mwingine hutazamwa kama suala la usawa katika dunia nzima na haki katika uchumi, popote inapotajwa inaashiria msimamo wa jumla wa kuukataa ubaguzi wa watu kwa misingi ya madaraja, jinsia ya mtu, kabila lake au utamaduni wake. Katika mtazamo wa vyama vya kijani, tofauti za watu kwa kile walichonacho zinasababishwa na kutokuwepo kwa taasisi za kijamii zenye kudhibiti dhuluma ya wenye nguvu dhidi ya walio wanyonge.&lt;br /&gt;Kwa ujumla vyama vya kijani vinaitafsiri haki ya kijamii kuwa ni kanuni inayosisitiza kwamba watu wote wanastahili mahitaji ya kimsingi ya mwanadamu bila kujali tofauti zinazoendekezwa, yaani kutofautiana kiuchumi, madaraja ya watu, jinsia, rangi, asili, uraia, dini, ulemavu au uzima wa maungo ya mwili. Haki ya kijamii ni pamoja na kufuta umaskini na ujinga, na kuwa na huduma bora za jamii kwa kila mmoja.&lt;br /&gt;Haki ya kijamii ni ainisho la kifalsafa la haki, yaani kuwapa mtu mmoja mmoja au kikundi cha watu kile wanachokistahili ndani ya jamii walimo.&lt;br /&gt;Dhana ya haki ya jamii imewavutia wanafalsafa tangu mwanafalsafa mkongwe Plato alipowakemea wanafalsafa chipukizi kutokana na madai yao kwamba haki maana yake ni chochote kile ambacho mwenye nguvu angeamua kiwe.&lt;br /&gt;Mdahalo wa kifikra umedumu hata leo kuhusu kutumia vigezo vya jumla au la vya kutambua kama kuna haki ya kijamii au kigezo cha nani mwenye nguvu na nani hana.&lt;br /&gt;Katika kitabu chake cha Republic Plato aliweka rasmi hoja yake kwamba jamii/dola iliyo barabara kabisa inaegemea kwenye nguzo nne za thamani, yaani;&lt;br /&gt;i/ Hekima&lt;br /&gt;ii/ Ujasiri&lt;br /&gt;iii/ Udhibiti&lt;br /&gt;iv/ Haki&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Vilevile, dhana ya haki ya jamii inatazamwa katika namna mbili.&lt;br /&gt;(a)      Haki ya jamii inayomaanisha usawa katika jamii hususan linapokuja suala la kugawana mavuno na majukumu na hivyo hoja hii hutumiwa katika siasa kuzungumzia hoja ya gawio na haki sawa&lt;br /&gt;(b)     Haki ya jamii ni hoja inayoonekana kutumiwa zaidi katika siasa za mrengo wa kushoto ikilinganishwa na inavyotazamwa katika mrengo wa kulia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Haki ya jamii inapata mamlaka yake kutoka katika vigezo vya maadili yanayoheshimiwa katika jamii husika.&lt;br /&gt;Hakika haki ya jamii ni dhana pana, lakini katika lugha rahisi haki ya jamii inaakisi namna ambavyo haki za binadamu zinadhihirika na kutekelezwa katika maisha ya kila siku ya watu na katika viwango vyote vya maisha ndani ya jamii.&lt;br /&gt;Haki ya ni chimbuko la changamoto ya hoja ya kuwapa watu wote fursa sawa na haki katika namna ambayo ni ya kweli na dhahiri. Hakika watu wote wana haki ya kushiriki kikamilifu ndani ya jamii.&lt;br /&gt;Jamii yenye haki itachukua hatua dhahiri za kuwalinda wanyonge na itanuia kwa dhati kuondoa visababishi vya umaskini na masaibu mengine yanayowakwaza watu wengi wasifurahie maisha na wasitumie uwezo waliojaaliwa kikamilifu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;SEHEMU YA TISA&lt;br /&gt;HAKI YA JAMII NA HUDUMA ZA JAMII&lt;br /&gt;Haki ya jamii na Elimu&lt;br /&gt;Haki ya jamii ni jambo la msingi kabisa kwa ajili ya Elimu bora (Connell, 1993). Kama mfumo wa jamii utawatendea visivyo haki baadhi ya wanafunzi katika jamii hiyo, ubora wa elimu ni wazi utakuwa na kasoro kubwa. Connell(ibid) anapendekeza uwepo wa mitaala ambayo mizizi yake imejikita katika haki na demokrasia. Mitaala hiyo iwe na uwezo wa kufungua fikra za wanyonge ili kuweza kifikia usawa katika jamii husika.&lt;br /&gt;Katika elimu, kama ilivyo katika taasisi nyinginezo za huduma za jamii mamlaka yote yamefungamana na haki.&lt;br /&gt;Wazazi, watoto, viongozi wa kisiasa na jamii kwa ujumla wana matarajio ya ni kitu gani shule zikifanye na ni jinsi gani kifanyike ili kufanya maisha ya mwanadamu yawe bora.&lt;br /&gt;Wengi huitazama shule kama taasisi ambayo mazao yake hayana budi kuujenga uchumi na kuiboresha jamii. Shule hususan za umma zipo kwa ajili ya kutumikia na kujenga maslahi ya umma nay a mtu mmoja mmoja.&lt;br /&gt;Masuala ya usawa na demokrasia ni miongoni mwa mambo yanayopewa kipaumbele na mfumo haki wa kijamii.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ujenzi wa Haki ya kijamii kupitia Elimu&lt;br /&gt;·        Sharti pawepo vipengele vya kujenga haki ndani ya mitaala&lt;br /&gt;·        Kuwepo kwa mipango ya kielimu ya kujenga mfumo haki (Education for Justice Programs; EFP)&lt;br /&gt;·        Kuwezesha uwepo wa fursa kwa wanafunzi kushiriki katika matukio na vitendo vinavyolenga kujenga Elimu ya Haki ya Kijamii.&lt;br /&gt;·        Ziwepo njia za ufundishaji darasani zinazotoa fursa kwa wanafunzi kujadili kanuni za haki katika Ulimwengu wa sasa.&lt;br /&gt;·        Masomo ya uraia/sayansi ya siasa yalenge kujenga ufahamu wa vitendo vilivyo kinyume na haki na ni jinsi gani watawala wanapaswa kijenga haki.&lt;br /&gt;·        Elimu ijenge fikra na mitazamo kuntu kuhusu masuala ya jamii, ukoloni, ubaguzi wa rangi, haki za binadamu, umaskini na mengineyo.&lt;br /&gt;·        Elimu isisitize na kuamsha tabia ya kujali haki za wanyonge katika jamii, yaani maskini, walemavu, makabila madogo, wanawake, watoto, ambao hawajazaliwa, na mataifa madogo katika Ulimwengu wa ushindani kiuchumi.&lt;br /&gt;·        Elimu isaidie kujenga maadili mahali pa kazi, uhusiano mwema baina ya mwajiri na mwajiriwa, mtumishi na mtumishi mwenzake, mtoa huduma na mteja n.k&lt;br /&gt;·        Elimu iongoze jitihada za ujenzi wa haki ndani na nje ya darasa.&lt;br /&gt;·        Elimu ifundishe kanuni za gawio haki na stahili ya kila mmoja.&lt;br /&gt;·        Elimu ijenge mazingira ya usawa wa kijinsia, iendeleze wasichana kwa kuwapa fursa katika michepuo yote ya sayansi asili na sayansi ya jamii.&lt;br /&gt;·        Elimu iwe ya fursa sawa kwa wote.&lt;br /&gt;&lt;a name="Social_Justice_Movements"&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;SEHEMU YA KUMI&lt;br /&gt;MFUMO SHERIA ZITENDAZO HAKI (JUST LAWS)&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Chini ya itikadi ya haki, sheria zote katika nchi sharti zizingatie haki za binadamu na viumbe hai wengine. Sheria zote sharti zipimwe kwa viwango vya haki kama zinavyozingatiwa na katiba ya nchi na katika miafaka/ matamko ya kimataifa.&lt;a name="External_links"&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;a name="Notes"&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;a name="References"&gt;&lt;/a&gt;REJEA&lt;br /&gt;&lt;a title="Carroll Quigley" href="http://en.wikipedia.org/wiki/Carroll_Quigley"&gt;Quigley, Carroll&lt;/a&gt;. (1961). The Evolution Of Civilizations: An Introduction to Historical Analysis. Second edition 1979. Indianapolis, IN: Liberty Fund.&lt;br /&gt;Rawls, John. (1971). A Theory of Justice, Cambridge, MA: Belknap Press of Harvard University Press.&lt;br /&gt;Rawls, John. (1993). Political Liberalism. New York: Columbia University Press (The John Dewey Essays in Philosophy, 4)&lt;br /&gt;Gad Barzilai, Communities and Law: Politics and Cultures of Legal Identities. Ann Arbor: University of Michigan Press.&lt;br /&gt;Philomena Cullen, Bernard Hoose &amp;amp; Gerard Mannion (eds.), Catholic Social Justice: Theological and Practical Explorations, (T. &amp;amp;. T Clark/Continuum,2007)&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt; &lt;/div&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/6014809184859864743-9200120126399652056?l=georgekahangwa.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://georgekahangwa.blogspot.com/feeds/9200120126399652056/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=6014809184859864743&amp;postID=9200120126399652056' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/6014809184859864743/posts/default/9200120126399652056'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/6014809184859864743/posts/default/9200120126399652056'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://georgekahangwa.blogspot.com/2008/02/haki-huinua-taifa.html' title='HAKI HUINUA TAIFA'/><author><name>Kahangwa</name><uri>http://www.blogger.com/profile/07414631690002879283</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='32' height='24' src='http://bp3.blogger.com/_3R2qky2qHsg/R9AwRuFfYjI/AAAAAAAAAAM/4OhJy7kgqsE/S220/george.jpg'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-6014809184859864743.post-1715930595887463890</id><published>2008-02-18T08:53:00.000-08:00</published><updated>2008-02-18T08:57:13.503-08:00</updated><title type='text'>PASAKA YA TANZANIA HAIJAJA  BADO</title><content type='html'>&lt;div align="justify"&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mjadala kuhusu Pasaka ya Tanzania miongoni mwa watanzania umeanza kwa utani, kwa watu kutumiana ujumbe mfupi wa simu wakilinganisha yaliyoyokea enzi za Yesu nyakati za mateso yake na yale yaliyojiri hivi karibuni nchini kwetu. Lakini kadri siku zinavyopita, naona mjadala huo unachukua sura ya hoja za kimantiki zaidi. Katika mazingira hayo nimeona niuchangie kwa undani, hasa hasa nikijaribu kutafakari kama pasaka yetu kama taifa la watanzania imekwisha kuwadia au la. Ninaukita mchango wangu katika hilo kwa kurejea matukio ya hivi karibuni (Mwezi Februari 2008) ya kuvunjwa kwa baraza la mawaziri na kuundwa kwa jingine tulilonalo sasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Moja ya mambo yanayotaniwa katika dhana hii ya pasaka ya Tanzania ni Kujiuzulu kwa aliyekuwa waziri mkuu baada ya kutolewa kwa ripoti ya Richmond. Binafsi naamini tukio hilo si ishara halisi ya pasaka yetu kwa kuwa kujiuzulu kwake hakukuwa kwa maslahi ya taifa ila kwa kiasi kidogo sana. Yamkini ni kwa maslahi ya chama chake kwa mujibu wa maneno yake mwenyewe, na kwa kuwa hasira ya Tanzania ilikuwa inazidi kuwaka, chama tawala (na serikali yake) kilikuwa hatarini. Kwa maneno yake mwenyewe Mheshimiwa alisema;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;"Mheshimiwa Spika, nimetafakari kwa niaba ya chama changu, kwa niaba ya Serikali yangu nimeamua kumwandikia Rais barua ya kumwomba niachie ngazi"&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kadhalika kuundwa kwa baraza ‘jipya’ hakuna upya wa maaana. Yamkini ni kwa maslahi ya chama kilichounda serikali hiyo. Uthibitisho mmojawapo wa hili  ni hitimisho alilolitoa mwenyekiti wa chama hicho baada ya kutusomea watanzania baraza aliloliteua aliposema;&lt;br /&gt;"Ahsanteni sana, kidumu chama cha mapinduzi"&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Angalia mwandelezo wa kurithishana madaraka katika baraza la sasa kama vile tuna utawala wa koo za kifalme, Msuya ndani, Mwinyi twende, na Malima haya. Bado wanaendelea kuteuana. Ni yale yaleee ya&lt;br /&gt;Wasikilizaji mpira sasa anao Kenyatta, Kenyatta anatoa pasi kwake Moi, Moi, Moi, anatumia mbinu za uprofesa wa kisiasa anatoa pasi ndefu kule kumtafuta Uhuru Kenyatta, lakini anatokea pale nambari moja wa timu ya NARC na kuunyaka mpira ule.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hapa nakumbuka pia mojawapo ya hotuba za mwisho mwisho za mzee Ruksa wakati wa utawala wake.  &lt;br /&gt;Aliwahi kusema kwamba katika utawala wake alijitahidi kuwashirikisha vijana, akatoa mfano wa JK na EL (asomaye na afahamu, kwa nini leo hii Mwinyi ni waziri)&lt;br /&gt;Baraza jipya bado si serikali ya timu ya ushindi, si timu ya Taifa, ni timu ya klabu iliyoongoza ligi kuu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kimsingi pasaka ya Tanzania kisiasa, kiuchumi na kijamii haijaja bado. Swali kuu la kujiuliza: Pasaka ya Tanzania itakuja lini na itakujaje? Hapo ndipo wasomi mliobobea, wajuvi wa nadharia na wenye exposure pana ya mambo, uzoefu na maono ya mbali mchanganue na kutafuta majibu&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Neno pasaka lina asili katika utamaduni wa wana wa Israel wa kumchinja kondoo kwa ajili ya ondoleo la dhambi.&lt;br /&gt;Utaratibu huo waliutumia pia wakati wakiwa utumwani Misri, ikabidi wamchinje mnyama na kupaka damu yake mlangoni ili malaika wa Bwana atakapopita awatambue na hivyo kuwaepusha adhabu iliyolengwa kwa mabwana wa watumwa.&lt;br /&gt;Katika kipindi hicho basi, pasaka ikamanisha kuondolewa katika utumwa wa Misri na kuwekwa huru kabisa, tena kwa kuhamishwa na kupelekwa katika nchi inayotirirka maziwa na asali, aliyoahidiwa baba yao Ibrahim.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Enzi za Bwana Yesu (Issa bin Mariam?), aligeuzwa yeye kuwa kondoo wa pasaka kwa kuuawa msalabani ili Taifa la Israel pamoja na mataifa mengine (of course wale wanaoamini hivyo) wakombolewe kutoka utumwa wa dhambi ambamo bwana wa watumwa ni Ibilisi mwenyewe, waingie katika uhuru wa Yesu na hatimaye katika uzima wa milele, katika nchi mpya, miji mipya (Yerusalem mpya) na mbingu mpya. Heri ni kwa wale waliojitakasa. Kuwepo huko kwa nchi mpya kutamaanisha uwepo wa mifumo sahihi ya maisha miongoni mwa wateule, ilihali mbingu mpya maana yake ni uwepo wa utawala bora kabisa (tafsiri ni yangu,  na si ya kitheologia)&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Basi pasaka ya Tanzania itakapowadia, itavaa sura zinazofanana na hayo. Tutaondolewa (tutapasaka- Passover) kutoka katika utumwa na mizigo ya ufukara na ufisadi inayolielemea Taifa kwa sasa na tutaingia katika enzi ya uhuru wa kimaisha sote! Wakati huo tutaiona faida halisi ya kuzaliwa katika nchi nzuri ya Tanzania inayofuka maziwa na asali (maliasili) mengi pengine kuliko hata Israel yenyewe ya huko mashariki ya kati. Tutakuwa na miji mipya na vijiji vipya ( hata kule kunakoitwa madongo poromoka patakuwa papya na penye hadi ya kuishi watu)&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati huo uchumi utarejeshwa mikononi mwa watanzania wenyewe na si kushikiliwa na wageni kama ilivyo sasa.&lt;br /&gt;Wakati huo akina mama wajawazito hawatalala tena mzungu wa nne kule Amana (na kwingine). Tunaowauguza hawatakufa kwa kukosa dawa, watoto hawatazaliwa tena pembeni mwa njia eti kwa sababu baikeli iliyombeba mama imeharibika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati huo kilio hakitasikika kusini, kaskazini, Mashariki wala magharibi mwa nchi yetu cha watoto wa kitanzania wanaoshindwa kwenda shule kwa sababu wazazi wao hawana pesa au serikali yao inatoa mikopo kwa wachache (chini ya 1% ya rika lengwa!). wala hatutasoma tena katika magazeti na blogi habari ya shule moja wanafunzi 400 mwalimu mmoja, ilhali kwingine walimu wapo hadi wa ziada.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mr. Ebbo (mwimbaji wa Bongo flava) hatamwogopa tena traffic police, eti hata akimwona kwenye TV ya nyumbani anastuka, kwa maana tutakuwa tumazipasaka enzi za rushwa barabarani, rushwa maofisini, rushwa mahakamani na kwingineko. Kwa maana licha ya mfumo tutakaokuwa tumeuanzisha kuwatiisha na kuwaogofya kabisa watoa na wapokea wa rushwa, watakuwa hawalazimiki kuichukua kwani mioyo yao imejengewa uadilifu sasa na wale wanaopokea rushwa ili waweze kumudu maisha hawatakuwepo tena maana maslahi ya kazi zao yanawatosheleza.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati huo kutofautiana kwetu kiufuasi wa vyama vya siasa hakutakuwa sababu tena ya kubaguana, bali kutageuka kuwa kichocheo cha maendeleo ya hali ya juu ya nchi yetu.&lt;br /&gt;Enzi hizo wenye dhamana ya uongozi watawaheshimu sana waliowapa dhamana hiyo (waongozwa) kwa maaana  ndio waajiri wao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lo! Pasaka ya hivyo itakuja kweli? Ni swali ambao mtu aweza kujiuliza.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pasaka hiyo itakuja siku ile tutakapokubali kubadilisha kabisa mifumo tuliyonayo kwa sasa na kuanza kufuata mifumo yenye maslahi dhahiri kwa Taifa letu.&lt;br /&gt;Katika suala la kubadilisha mifumo, wapo wanaoona hilo lianze kwa kubadilisha katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Katiba tuliyonayo sasa, imepigiwa kelele sana kwamba inaendekeza uwepo wa mfumo wa chama dola badala ya kukifanya chama kilichoko madarakani kiwe chama cha siasa na si vinginevyo. Watawala wa sasa hawataki hilo libadilike maana linawahakikishia kuendelea kutawala ( ndio maana mara kadhaa wamejitapa wakisema kuwa watatawala milele). Kiburi chote hicho kinatoka kwenye katiba yetu wenyewe.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hakika pasaka yetu haiji hadi hapo katiba itakapoondokana na mfumo huo. Itakaporuhusu, matharani uundwaji wa serikali ya umoja wa kitaifa badala ya serikali ya chama tawala. Itakapotenganisha waziwazi mihimili mikuu ya dola, mfano wabunge wakabaki kuwa wabunge na mawaziri wakawa ni wateule wa mkuu wa dola kwa mujibu wa wasifu wa kila mmoja wao na wakatibitika hivyo mbele ya bunge.&lt;br /&gt;Katiba yetu pia haina budi kachana na kutuadaa kwamba tuko katika mfumo wa kijamaa( kumbe yale mazishi yaliyofanyika Zanzibar, ulizikwa mfumo gani wa uchumi, kumbe hizi sera za ubinafsshaji na uwewkezaji wa kigeni ni za mfumo gani wa uchumi?)&lt;br /&gt;Lakini hapa nachelea kumpigia mbuzi ngoma ya kihaya. Nakumbuka katika miaka ya tisini wasomi wa chuo kikuu mlimani (sio wote) walianzisha jitihada iliyojulikana kama National Committee for Constitutional Reform (NCCR), iliyolenga kuhakikisha kwamba ama tunakuwa na katiba mpya au iliyopo inafanyiwa marekebisho ya haja, lakini watu walipoanza kuonjeshwa ‘atamu’ za ujumbe wa halmashauri kubwa na uanakamati katika kamati ya wenye shingo nene (NEC) waka declare the co- mission futile na wakai- abandon.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mfumo mwingine ambao hatuna budi kuubadili ili kuruhusu pasaka yetu ije ni Mfumo wa kiutendaji/ kiutawala kutoka ngazi moja hadi nyingine. Mawakili wetu katika eneo hili wanapenda kusisitiza haja ya Genuine Decentralization. Ingawa Tanzania tunadai tumepeleka madaraka ngazi za chini, kwa kuwa tuna halmashauri za wilaya na serikali za vijiji, tena eti tunatumia mikakati shirikishi katika uandaaji na usimamizi wa mipango ya maendeleo, mambo hayajakaa sawa. Utawala wa juu licha ya kwamba bado unazinyima autonomy mamlaka hizo za chini, bado mahusiano ya serikali kuu na serikali za mitaa yanaendekeza urasimu usiokuwa wa lazima.&lt;br /&gt;Nitoe mfano, alipotutangazia baraza jipya Mheshimiwa Rais alisema anaunganisha masuala ya Elimu yashughulikiwe na Wizara moja. Lakini ki muundo bado sio hivyo. Hiyo TAMISEMI (ambayo binafsi sipendi iwepo) bado ina mkono wake wa kirasimu katika masuala ya elimu huko ngazi za chini. Tena nadhani kwa sasa hali itakuwa mbaya zaidi, maana Halmashauri zimepewa hata elimu ya sekondari ( kwa maana hiyo TAMISEMI imejitanua sasa kutoka elimu ya msingi hadi hata ya sekondari, si ajabu pasaka yetu ikichelewa zaidi utasikia na vyuo vya ualimu navyo)&lt;br /&gt;Hili linanikumbusha enzi zile za ualimu wangu wa katika shule za msingi, tulimlilia Rais wa chama chetu wakati huo Mhe. Mama Margareth Sita, tukiomba masuala yetu yashughulikiwe na chombo kimoja, maana tulikuwa tukishindwa kuelewa, unapata tatizo unaambiwa nenda wilayani, mara hili ni la Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC), mara hapa ukawaone watu wa mkoani, nako uaambiwa labda uende TAMISEMI Dodoma, unafika huko nako wanakusukuma wizarani Dar es Salaam, ili mradi ni mgongano tu wa majukumu na hiyo kero kubwa kwa mwenye kuhitaji kuhudumiwa ili naye akawahudumie wengine.&lt;br /&gt;Tulilia sana walimu wa wa shule za msingi, wengine waliolewa, wakashindwa kuhama kutoka katika Halmashauri zinazowaajiri kuwafata wenzi wao waishio katika wilaya tofauti. Basi hayo yakawapata walimu wa msingi, sasa wameingizwa huko huko walimu wa sekondari.&lt;br /&gt;Yamkini, kuzungumzia walimu ni mtazamo wa upande mmoja. Upande mwingine ni suala zima la ubora wa elimu chini ya mamlaka ya TAMISEMI kwa mgongo wa halmashauri. Tunasema tena tunaamini, kwamba kila mtoto wa taifa hili ana haki ya kupata elimu bora, kwa maana hiyo asome katika shule bora, zenye walimu bora, mitaala bora na vifaa bora vya kufundishia. Nasikitika chini ya mamlaka na muundo wa sasa hilo halitawezekana (pasaka bado) . kitakachotokea halmashauri/ manispaa za miji zitaendelea kuwa na umiliki wa walimu wa kutosha katika sekondari na praimari, ilhali kule vijijini taabu na mashaka makubwa yataendelea. Kwa maana itakuwa sasa kwamba si rahisi tena mwalimu aliyeajiriwa na manispaa ya Kinondoni akahamishiwe (wapi kule ambako hakuna barabara na hivyo Rais hajawahi kufika?)&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mfumo mingine wa kubadili ni CCM, ni ama chama hicho kioge kwa damu ya mwana kondoo ili kiwe safi kama theruji ya Finland, au kitoke madarakani sasa (kwani kitafia madarakani?) Hapa natahadhari kidogo ugomvi wa kisiasa maana najua katika nchi yetu kuna wana CCM si haba. Jamani, Baba wa Taifa, mhasisisi wa chama hicho si alisema kiko kama kokoro, sasa kwa nini tusione haja ya chama hicho kuoga? Jamani, mmoja wa waliowahi kuwa makatibu wake wakuu (Marehemu Kolimba) si alisema hakina dira, sasa haja ya kuitafuta dira sahihi itakosaje? Mnh, Wapinzani nao (sijui wanampinga nani – wamepewa jina baya!) si walisema wakati fulani kwamba kashfa ya BOT ni ya CCM moja kwa zote, kwa kuwa mafwedha yaliyochotwa huko yalimwagwa kwenye kampeni za kisunami za chama hicho mwaka 2005. We ngoja Dr. Balali arudi, huenda akatufungulia njia ya pasaka yetu kwa kusema ukweli wote ( hivi na yeye alitolewa kafara kama mwana kondoo wakati huenda maskini dhambi si yake?)&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mfumo mwingine wa kubadili ni utaratibu wetu wa kuwalea na kuwaibua viongozi. Nashawishika kusema kwa sasa utaratibu huo kama upo hauna tija wala ufanisi, na si ajabu haupo kabisa. Tunapolia leo kwa kukosa viongozi waadilifu, tumlaumu mama mlezi na tumlazimishe basi arekebishe staili yake ya ufundaji. Katika hilo vyuo vyetu vinaguswa. Hey, Universities and other higher learning institutions, how do you nurture the future leaders of the nation?&lt;br /&gt;( Niliwahi kumsikia Prof. Mmoja akijivunia utendaji wa Mhe. Zitto, akaongeza kusifia kwamba ni zao halisi la Mlimani. Na sasa nimesikia hapo mlimani kuna wanaojivunia umwenzetu wa Dr. Mwakyembe) Binafsi namkumbuka Zitto akiwa mwanafunzi mwenzangu UDSM, tulifahamiana kwa karibu kwenye mambo ya uongozi wa wanafunzi. Nasikitika ukweli ni kwamba malezi ya kiuongozi aliyopewa na mlimani yalilenga kumdumaza. Mara kadhaa alisimamishwa masomo. Nakumbuka siku moja nikiwa nazungumza naye chumbani kwake, walikuja watu wa ofisi ya Mwadili wa wanafunzi, wakamtaka aondoke chuoni mara moja kwa kuwa wanamtuhumu kupanga njama za mapinduzi ya serikali ya DARUSO (chama cha wanafunzi).&lt;br /&gt;Nasikitika kwamba wakati huo badala ya chuo kulea kipaji chake cha uongozi na uthabiti katika misimamo, kilim- intimidate mara nyingi. Well, hayo yalimpata Zitto, waliopo sasa chuoni hapo wanalelewaje, au wanafundwa kuukubali mfumo wa kifisadi tena kwa namna ya kitiifu ya yours faithfully.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ipo pia mifumo mingine ya kubadili, wakati ukiruhusu tutaijadili pia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pasaka yetu itakapowadia,Mwanakondoo wa pasaka ya Tanzania, hatutamchinja physically, ila itamlazimu kuitoa kafara nafsi yake (maslahi yake binafsi, ya familia na ukoo wake) ili ayatumikie tu maslahi ya Taifa. Jukumu letu la pamoja ni kumtambua mwanakondoo huyo ili tuchinje kula pasaka yetu mapema zaidi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pasaka ya Tanzania itakuja,haijaja, itakuja lini? Watanzania tutafakari na kuamua sasa.&lt;br /&gt;  &lt;/div&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/6014809184859864743-1715930595887463890?l=georgekahangwa.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://georgekahangwa.blogspot.com/feeds/1715930595887463890/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=6014809184859864743&amp;postID=1715930595887463890' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/6014809184859864743/posts/default/1715930595887463890'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/6014809184859864743/posts/default/1715930595887463890'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://georgekahangwa.blogspot.com/2008/02/pasaka-ya-tanzania-haijaja-bado.html' title='PASAKA YA TANZANIA HAIJAJA  BADO'/><author><name>Kahangwa</name><uri>http://www.blogger.com/profile/07414631690002879283</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='32' height='24' src='http://bp3.blogger.com/_3R2qky2qHsg/R9AwRuFfYjI/AAAAAAAAAAM/4OhJy7kgqsE/S220/george.jpg'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-6014809184859864743.post-4862435991038001183</id><published>2008-02-17T13:07:00.000-08:00</published><updated>2008-06-18T07:35:05.229-07:00</updated><title type='text'>CHANZO KIKUU CHA UMASKINI WA TANZANIA</title><content type='html'>&lt;div align="justify"&gt;&lt;strong&gt;CHANZO KIKUU CHA UMASKINI WA TANZANIA&lt;/strong&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Miaka nenda miaka rudi, taifa la Tanzania limeeendelea kuhesabika miongoni mwa nchi maskini kabisa duniani. Sio tu kuhesabika uko kwa taifa hili kuko katika takwimu za wataalamu wa uchumi, bali pia kiwango cha maisha ya watanzania wengi ni cha chini sana. Watanzania tumeeendelea kuishi maisha ya dhiki sana, mulo kwa wengi kuupata imekuwa taabu, nyumba wanamoishi watu ni hohehahe, elimu ya wengi wetu ni duni, kusafiri toka sehemu moja hadi nyingine shida tupu (vijijini na mijini), huduma za afya licha ya kutopatikana kwa urahisi, zilizopo wanaomudu gharama zake ni wachache na hata hivyo hazilidhishi, vipato vya wafanyakazi, wakulima na wafanyabiashara viko hoi, ili mradi tu ni dhiki juu ya nyingine.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati walio wengi taabu zetu kwa kutaja chache ndio hizo, wapo wenzetu wachache nchini ambao maisha yao ni ya neema, tena neema tele. Watanzania tumeendelea kujiuliza, kulikoni bila majibu. Baadhi yetu tu, mfano wasomi na wengine, wamejaribu kutafuta majibu na ufumbuzi wa umaskini huu lakini hadi sasa bila suluhisho.&lt;br /&gt;Kwa kutumia nadharia kwa mfano, wapo wanaosema chanzo na kiendelezo cha umaskini wetu, ni tabia ya watanzania wengi kutojiwekea akiba, yaani baada ya kuzalisha kidogo, kidogo hicho chote kinawekwa katika matumizi, hivyo hakuna akiba na kwahiyo hakuna uwekezaji katika mradi wowote mpya wa uzalishaji au kupanua uliopo, na matokeo yake uzalishaji unaendelea kuwa kidogo kama sio kupungua, ilimradi unakuwa ni mduara tatizi usiokoma wa ufukara. Kwa kusimamia kwenye nadharia hii, wapo wanaotuhubiria watanzania kwamba tujenge tabia ya kuweka akiba jamani. Ni mahubiri mazuri sana, lakini swali la kujiuliza hapo ni je, kweli kuna mtanzania asiyetaka kuweka akiba? Kwa maoni yangu, mtanzania wa hivyo hajazaliwa, bali sisi tunaoishi roho zetu zi radhi kuweka akiba lakini hali halisi inakataa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wengi watakubaliana nami kwamba, mfanyakazi wa Tanzania ya leo ambaye mara nyingi mshahara wake wa mwezi huisha siku kumi au kumi na tano baada ya kuupokea, kumwambia aweke akiba ni kumkejeli mchana kweupe! Mfanyakazi wa kitanzania, maisha yake yamejaa madeni kwenye maduka ya rejareja. Laiti kama mikopo anayochukua kwenye maduka hayo ingekuwa ya bidhaa za ziada, sio, ni madeni yatokanayo na mahitaji ya sukari, chumvi, sabuni, sembe na bidhaa nyingine za namna hiyo.&lt;br /&gt;Kilio cha wafanyakazi hawa kimeendelea kuwa ni kile kile mwaka hadi mwaka, wakidhani tatizo ni kwamba mshahara hautoshi. Watawala wetu katika kujibu malalamiko ya mishahara kutotosha, wamekuwa wakifurahisha mikutano wanayoihutubia kwa kuimba ngonjera ile ile, ‘Mwaka huu wa bajeti tutaongeza mishahara’ mara kadhaa wanaongeza kweli. Nyongeza hizo licha ya kuwa kiduchu zimeendelea kutotatua tatizo, bado mshahara hautoshi na hauelekei kama utatosha siku za karibuni.&lt;br /&gt;Kumbe shida ni nini hasa? Wengine wakasema ni kwa sababu kuna mfumko wa bei, kiasi kwamba nyongeza inapotoka tayari bidhaa madukani zimepanda mara dufu na huduma za jamii zimeenda juu vile vile.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa upande mwingine yapo madai kwamba umasikini wetu pengine unatokana na uvivu wa watanzania (hili linasemwa sana na wabaguzi ambo mara kadhaa wamedai eti sisi waafrika ni wavivu). Bado naendelea kujiuliza kama hilo lina chembe zozote za ukweli, ili kama hilo ndio tatizo la Tanzania, tusione aibu kulikiri na hivyo kuamua kuondokana nalo. Lakini haiingi akilini kirahisi kwamba watanzania tunaofanya kazi kutwa kucha, usiku na mchana, siku za kawaida, mwisho wa wiki na hata kwenye sikukuu hadi wengine tunaitwa walalahoi, bado tunaweza kuambiwa uvivu ndio sababu ya umaskini wetu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Maeneo ya vijijini, mkulima masikini anamka kabla ya jogoo kuwika ili awahi shambani, inamlazimu wakati mwingine kushinda njaa ili asirejee nyumbani na kuharibu kazi aliyokusudia kuimaliza siku hiyo. Msimu wote wa kilimo, mvua yake, jua kali lake na taabu nyinginezo za maporini. Maskini mkulima huyu kapinda mgongo na jembe lake la mkono ili mkono uende kinywani. Tena anapaswa alime kwa bidii hata mazao ya biashara ili apate fedha, maskini mazao yake miaka nenda miaka rudi hayapati bei inayolingana japo angalau na nguvu kazi yake aliyotumia. Bado mtu huyu aambiwe wewe ni maskini kwa sababu ya uvivu?&lt;br /&gt;Kadhalika kwa wafanyakazi, nitolee mfano wetu sisi walimu; mwalimu anayedamka asubuhi na mapema sambamba na wanafunzi wake, akafanya kazi zake siku nzima ya kazi, na kwa kuwa hazikuisha akabebana nazo kwenda nyumbani, ili usiku awashe kibatali na kuzimalizia (hana tofauti na Kayumba), baada ya hapo aandae anafundisha nini kesho, wakati wanafunzi wake wako likizo yeye ndio kwanza anasahihisha mitihani yao na kuandaa mpangokazi wa muhula unaofuata. Huyu naye aambiwe sababu ya umaskini wake ni uvivu, kweli?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Aidha upo mtizamo kwamba, sababu ya kuendelea kwetu kuwa masikini ni kwa kuwa watanzania tunamiliki mali lakini hazina urasmi, yamkini wa kutuwezesha kupata mikopo toka taasisi za fedha na kadhalika. Ndio maana ukaja huu makakati wa kurasmisha mali hizo kama harakati mojawapo ya kupambana na ufukara nchini. Sambamba na hilo, ipo dhana ya kwamba mikopo kwa watu binafsi na vikundi vya jamii itatuokoa ufukarani. Kwa sababu hiyo sasa tuna mamilioni ya Kikwete na mikopo mingine!&lt;br /&gt;Maswali bado ni mengi hapo. Ni nini kinaweza kutokea kwa mfano, iwapo watanzania watachukua hiyo mikopo midogo midogo na hatimaye kugeuka taifa la wachuuzi, tena wa bidhaa zitokazo nje, umaskini utaondoka? Uchumi utakua? La hasha, maana bado mimi naamini kutokuwepo kwa mikopo hiyo bado sio sababu ya umaskini wa wananchi. Hata hivyo kuwepo kwake, si hatua ya kubeza.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika harakati za kutusaidia, tumeimizwa sana kuwekeza popote fursa inapojitokeza, mfano kununua hisa katika makampuni au mashirika. Hili limefanyika sana. Watanzania tunakumbuka pia Rais mstaaafu wa awamu ya tatu alivyotuhutubia siku moja, kwamba tofauti yetu na matajiri wa nje, hususan wanaokuja nchini kuwekeza ni kwamba waliona mapema umuhimu wa hisa, na kwa kuzinunua ndiko walikopata mitaji yao wanayoihamishia sasa nchini ketu ili wachume zaidi. Hivyo akatushauri tuone haja ya kununua hisa kama kweli tunataka kuondokana na umasikini. Lakini bado tunarudi kulekule, yule mwenye mshahara usiomfikisha mwisho wa mwezi, au ambaye mazao yake hayajanunuliwa na ambaye mwenye duka anamdai, kapata wapi cha kununulia hisa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tumeedelea kujiuliza zaidi na zaidi juu ya chanzo na suluhu ya umaskini wetu. Wapo wanaodhani kwamba sisi ni maskini kwa majaliwa ya maumbile. Sisi ni maskini kwa sababu taifa letu halikuumbwa tajiri kama yalivyo mataifa mengine. Hili ndio kwanza halina hata lepe la ukweli.&lt;br /&gt;Tanzania kwa asili ni nchi tajiri sana! Tena ingefaa watanzania tutambue na kujivunia ukweli huo kwamba nchi yetu imependelewa muno kuliko nchi nyingi sana duniani. Utajiri wetu wa maliasili hauna mfano. Tuna eneo kubwa sana la ardhi tena yenye rutuba, ifaayo kwa kilimo na shughuli nyinginezo za kiuchumi. Yapo mataifa ambayo watu wake si maskini kwa kiwango chetu, lakini ardhi yao waliyojaliwa ni jangwa. Hapo asomaye na afahamu ni kwa nini Namibia fedha yao ina nguvu sana ukilinganisha na ya kwetu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tanzania tumejaliwa madini na vito vya thamani vingi sana, na vingine havipatikani popote ulimwenguni ila Tanzania tu. Kuitaja Tanzanite kumezoeleka, watanzania tufahamu pia kwamba licha ya dhahabu, almasi, bati, taja madini yoote yang’aayo na yasiyon’gaa utayakuta nchini. Ni sisi pekee vile vile tuliojaliwa madini ambayo walioyagundua waliamua kuyaita Nyerereite kwa sababu ya upekee wake duniani.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kana kwamba hilo halitoshi, wakati wenzetu wanalia kwa kukosa maji, sisi kila mahali ni mito na maziwa makubwa yanayopendeza hata kwa mpangilio na mtandao wake nchi nzima. Ziwa kubwa kuliko yote Afrika liko Tanzania, Ziwa lenye kina kirefu kuliko yote Afrika nalo liko Tanzania! Ndio maana mojawapo ya nyimbo zetu za kizalendo tunasema, tazama ramani utaona nchi nzuri, yenye mito na mabonde mengi ya nafaka!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Aidha wakati mataifa mengine, yamefungiwa ndani kwa ndani kiusafiri, sisi tuna pwani ya bahari ya Hindi yenye kilometa nyingi za urefu na bandari kadhaa zinazotuhudumia wenyewe na mataifa jirani yanazitumia tena kwa kutulipa fedha nyingi tu za ushuru. Mshangao uaongezeka tunapoambiwa mataifa hayo hayo yanayotutegemea katika sekta hiyo, yanatuzidi kiuchumi.&lt;br /&gt;Tuseme nini kuhusu baraka ya misitu na wanyama na vivutio vingine vya utalii. Utajiri wetu katika eneo hilo umeyatia wivu mataifa mengi ambayo hayana, lakini mataifa hayo hayo watu wake si fukara kama sisi. Kulikoni?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Baba wa taifa Marehemu Mwalimu Julius Nyerere aliwahi kutueleza, tunahitaji watu ili kuiendeleza nchi yetu. Ingawa hitaji la watu si tu kwamba wawe wengi bali pia wawe na maarifa na maadili, sisi Tanzania tumejaliwa hata katika hilo. Jamani, kwa sasa twapata milioni arobaini (40), lakini nchi zenye wakazi kidogo tu zinatuzidi mbali kiuchumi. Unakuta nchi kwa ujumla ina idadi ya watu sawa na wakazi wa Dar es salaam peke yake au pungufu, lakini maendeleo yao hatuwafikii hata robo. Labda nidokezee tu kwamba, idadi ya wakazi nchini Finland kwa mfano, ni milioni tano na ushee kidogo. Namibia nilikotolea mfano wa kwanza, kuna watu wasiozidi milioni mbili. Tuseme nini basi, wingi wetu ndio unaotuponza? La hasha, ingawa kwa mtazamo mwingine idadi kubwa ya watu wasio na mwelekeo ni tatizo. Litupasalo sisi ni kuutumia vizuri wingi huo, kuuondoa katika umaskini ili kila mmoja wetu azidi kuwa wa manufaa kwa taifa.&lt;br /&gt;Mataifa mengine, yametumia wingi wao kupiga hatua kubwa sana kimaendeleo. Kinachotakiwa ni kuwa na watu walio bora, kwa maana ya wenye elimu, afya na uwezo wa kutenda. Umasikini umekuwa chanzo cha wananchi wetu kuwa na elimu duni na afya zisizolidhisha. Bahati mbaya baadhi ya waliobahatika kupata elimu nzuri wamekimbilia nchi za nje kwa sababu ya maslahi duni yanayotolewa hapa nchini. Tuna bahati mbaya kwamba watanzania wenzetu hao wametoa mchango mkubwa sana katika kutokomeza umasikini wa nchi za wenzetu, ilihali nyumbani (kama ulivyo msemo wa mitaani) kumedoda.&lt;br /&gt;Hoja yangu hapo ni kwamba, wingi wetu si chanzo cha umasikini bali ni baraka ambayo laiti tungeitumia vizuri, Tanzania ingehesabika katika ulimwengu wa kwanza.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mtazamo mwingine juu ya umasikini wetu, ni ule unaoona kwamba sababu zake si za ndani bali zinatoka nje. Mtazamo huu unauhusianisha umasikini na ukoloni tulioupitia katika historia ya nchi yetu. Kwamba kwa kutawaliwa na wakoloni wa kijerumani na baadaye waingereza, tulinyonywa na tunaendelea kunyonywa kupitia ukoloni mambo leo, utandawazi na uwekezaji wa kigeni. Hapa pana ukweli wa kiasi chake, japo hapatoshi kuwa sababu hasa inayoeleza chanzo cha ufukara nchini, na wala suluhu yake haitakuja kwa kupambana tu na mkoloni wa zamani na wa sasa. Mataifa kadhaa ulimenguni yalipitia kutawaliwa na wakoloni kama sisi, lakini leo hii wao (sio wote) si masikini kama sisi. Hapa nirudie mfano wa Finland iliyotawaliwa na Urusi na Sweden, au nchi za Asia zilizokuwa makoloni ya mwingereza. Walijikomboa kutoka ukoloni, wakakaa chini kizalendo wakajenga nchi zao, umaskini ukatokomea. “kwani wao waliweza wana nini, na sisi tunashindwa ni kwanini?”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata hivyo hatuwezi kupuuza hujuma za nchi zinazojifanya viranja wa ulimwengu, hususan nchi za magharibi dhidi ya nchi changa. Hawa hawa ndio wanaendelea kutuharibia kwa kutupangia nini tufanye na nini tuache. Wanaendelea pia kushirikana na wazandiki wasioitakia nchi yetu mema bali nafsi zao, japo ni watanzania wenzetu. Ndio hao aliowasema Baba wa taifa, kwamba ni miti (mipini) iliyomo kwenye mashoka ya chuma inayowakata akina miti. (shoka bila mpini halikati mti, ati) Hivyo, tunapoendelea kuulaumu/ kuusingizia ukoloni na utandawazi tusisahau kuwatazama Yuda Iskariote wetu. Wenzetu hao ni sababu mojawapo ya kudumu kwa umaskini wetu, na nadhani kwa kuwadhibiti tutaudhibiti umasikini vilevile.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati fulani nimepata kusikia baadhi ya viongozi wetu wakitaja kuwa, sisi ni masikini kwa sababu kadhaa, mojawapo ni vita tulivyopigana dhidi ya Idd Amin wa Uganda mnamo mwaka 1978/79 (miaka therathini imepita sasa) Mnh, binafsi sipuuzi athari za vita hiyo, lakini kuitaja kama sababu ya umasikini kukithiri nchini, ni kukosa kisingizio, kujisemea tu au kuogopa kujinyooshea kidole. Jamani, vita hiyo imepiganwa muda mrefu umepita sasa, tena ilidumu kwa miezi sita tu. Watasemaje majirani zetu wa Rwanda na Burundi ambao kwa sasa nchi zao (hasa Rwanda) zinatengemaa kiuchumi, na ajabu Faranga yao ina nguvu kuliko Shilingi ya Tanzania. Namibia wamepata uhuru mwaka 1990 jamani, vita vya ukombozi huko vilidumu kwa muda, ilihali sisi tulipata uhuru bila damu.&lt;br /&gt;Uhuru wetu wa bila kumwaga damu na utulivu wetu (wengine wanasema amani,amani umasikinini?) wa muda mrefu, zilikuwa ni sababu tosha za sisi kuwa mbali sana kimaendeleo kuliko wenzetu wengi. Mungu atupe nini ndugu zangu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wapo vile vile wanaosema, watanzania hasa vijana, ni maskini kwa sababu ya ukosefu wa ajira. Tatizo la ajira miongoni mwa vijana kweli lipo, lakini kimantiki halikupaswa kuwepo. Katika enzi hizi za sayansi na teknolojia, ambamo matumizi ya maarifa yameongezeka, nchi yetu inatajwa kuwa mojawapo ya nchi zisizo na raslimaliwatu yenye kumudu hayo. Hivyo tatizo si kwamba ajira hazipo, ila vijana hawana elimu. Nchi yetu vile vile inazo sekta ambazo wengi wanaoziendesha nguvu zao sasa zinaelekea machweo. Matharani sekta ya kilimo, kwa kuwa inaonekana kutokuwa na tija, vijana wanaikimbia na kuwaachia wazee vijijini. Laiti kama sekta hiyo ingebadilishwa sura yake ya sasa, wimbo wa hakuna ajira ungewekwa makumbusho. Laiti kama elimu ingetolewa kwa vijana wote hawa, tena elimu iliyo sahihi, Tanzania isingekuwa tena mahali ambapo mwekezaji kutoka nje anawakosa wenyeji wenye taaluma na ujuzi unaoendana na biashara/shughuli yake, inamlazimu kuja na wataalamu wake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Niliyoyajadili hapo juu, si mapya sana. Haja ya kuyataja inajitokeza kwa ajili ya kujenga mazingira ya hoja yangu kuu, na vile vile kulitazama suala la umasikini, chanzo chake na suluhu yake kwa mapana zaidi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Juhudi nyingi watanzania tumefanya, lakini umasikini umeendelea kusimama wima kama mlima Sayuni unaosemekana hautatikisika kamwe. Au kama Mbuyu katika mbuga za Dodoma. Tumefika mahali tumegundua kisababishi kikuu cha uamsikini wetu, na hicho ndio ninataka tukiangalie leo kwa makini ili hatimaye tuchukue hatua sahihi na mwisho umaskini nchini ugeuke historia ( tena isiyojirudia)&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika familia Fulani, wamejaaliwa mali nyingi walizorithi kutoka vizazi na vizazi. Wanafamilia waadilifu wanajitaidi kufanya kazi kwa bidii lakini wanashangaa mwisho wa siku kinachotoka jikoni, badala ya kuwashibisha ndio kwanza kinawaumisha njaa zaidi. Miaka hadi miaka wanaendelea kukondeana maskini hawa. Hatimaye wanajuliza, kulikoni huko jikoni? Mara lo, wanagundua wapishi ni wezi.&lt;br /&gt;Familia inakaa kikao cha dharula, agenda ni moja, WAPISHI ni WEZI. Hapo hakuna anayepindisha lugha, eti wapishi wamepungukiwa uaminifu, ooh tuna mashaka nao. Wote wameamua kuliita sepetu ni sepetu, wala sio kijiko kikubwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ndugu zangu, Tanzania ndio familia yetu, kisababishi kikubwa cha umasikini wetu, njaa yetu na matatizo mengine lukuki ni kwamba; TULIOWAPA DHAMANA YA KUSIMAMIA RASLIMALI ZETU NI WEZI.&lt;br /&gt;Siku za karibuni yametumika maneno mengi kuwasema, wangine wanasema ni MAFISADI, ni jina sahihi lakini halitoshi, pengine wanaitwa wala RUSHWA ni kweli lakini hawa ni zaidi ya wala rushwa. Msamiati mmoja rahisi ambalo hata mtanzania aliyeko darasa la kwanza hatahitaji kamusi ya Tuki kuuelewa … WEZI&lt;br /&gt;Wametuibia akiba zetu, wametuibia nguvu kazi zetu, wameiba jasho letu, wameiba mali asili zetu, wamewakaribisha wezi wenzao kutoka ughaibuni wakaiba na kuiba na kuiba isivyopata kutokea katika historia ya taifa letu, wakajitajirisha. Makazi yao yakawa majumba mithiri ya mahekalu, ilihali sisi wenye mali tunaishi mbavu za mbwa, usafiri wao ukawa mashangingi, VX, Lange Rover, Benz, BMW, ilihali sisi tunapougua tunasafirishwa kwa baiskeli mbovu. Watoto wa wenzetu wakaao mijini hawana usafiri wa kwenda shule, wakati watoto wao wanawatimulia vumbi la maprado. Lo, tulidhani utajiri huo ni zao la jitihada zao kumbe wizi, tena wizi usio na haya.&lt;br /&gt;Ndugu watanzania, tumasikia sasa vya kutosha juu ya wizi wa mabilioni uliotokea katika Benki yetu kuu. Fedha zilizoibiwa, katika kupitia akaunti ya mabeni ya nje (shilingi bilioni 133) na hata ambazo hatujatajiwa bado, kwa mahesabu ya haraka haraka, zingeweza kutatua tatizo la shule mbovu, zisizo na vifaa vya kufundishia wala walimu. Tangia sasa mtu asituambie tena kwamba matatizo yaliyoko katika elimu yanatokana na umasikini wa nchi. Tunaujua ukweli sasa, yanatokana na WIZI.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tumesikia pia habari za kusainiwa kwa mikataba mibovu, na ununuzi wa vifaa vibovu. Nisingependa kurudia kutaja IPTL, Richmond, Buzwagi, Ununuzi wa rada, Ndege ya Rais na mengine. Hawawezi tena sasa kutudanganya kwamba waliosaini mikataba hiyo walipungukiwa maarifa, la hasha, waliisaini KIWIZIWIZI.&lt;br /&gt;Tumeimbiwa sana nyimbo za mrahaba kichele unaolipwa na makampuni yanayochimba madini, na jinsi usafirishaji wa madini usivyoangaliwa kiasi kwamba inabidi eti kamati iende ng’ambo kuchunguza mchanga wa madini unaosafirishwa kwenda huko. Jamani, huu wizi kumbe umeenea ndani ya taasisi zetu na katika machimbo ya maliasili zetu, kila mahali!.&lt;br /&gt;Tunapoendelea kukosa huduma za afya, si kwamba nchi yetu ni masikini, bali wezi wanachota vifungu na mali ambazo zingeboresha huduma hizo.&lt;br /&gt;Tunapoendelea kupata ujira duni kwenye ajira zetu, si kwamba nchi yetu ni masikini, bali pato ambalo lingetumika kuboresha mishahara ya watumishi, WEZI wamelitia vinywani mwao.&lt;br /&gt;Tunapoendelea kuumizwa na kupanda kwa gharama za maisha, petroli juu, mchele juu, unga juu, umeme juu, sabuni juu, nauli juu; si kwamba nchi yetu ni masikini, bali kodi tunayolipa kupitia makato ya mishahara yetu, na kupitia bidhaa hizo hizo tuanzonunua, zinishia kwenye matumbo ya WEZI na washirika wao wa ndani na nje.&lt;br /&gt;Yamkini tunapoendelea kuwa na bejeti ya nchi inayotegemea misaada ya wahisani kwa asilimia arobaini (40%) si kwamba ni kwa sababu ya umasikini wetu, bali WEZI wanahujumu uchumi wetu.&lt;br /&gt;Tunapoendelea kuwa na barabara mbovu, makazi duni na kila aina za ufukara si kwamba sisi ni wavivu, hatuweki akiba au hatununui hisa. Si kwamba ni kwa kuwa tulipigana na Amin au kuna upungufu wa ajira, bali ni kwa sababu tuliowapa dhamana ya kusimamia utajiri wetu kwa manufaa ya wote wameamua kuwa WEZI waliokubuhu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Umefika wakati sasa tuwashughulikie wezi hawa wote, mmoja baada ya mwingine, bila kumwangalia nyani usoni ili tulinusuru taifa.&lt;br /&gt;Umefika wakati tuseme yatosha nyimbo za ulaghai tulizoimbiwa na wanasiasa waongo, maana ukweli sasa tunaujua.&lt;br /&gt;Hukumu yao isiwe ya sheria mkononi (ingawa ikitokea hivyo sitashangaa). Hukumu ianze kwa msaada wa vyombo vyetu vya sheria nchini, wakamatwe wote wafikishwe mahakamani, wasio na hatia wajulikane, WEZI wote ndani ikiwa ni pamoja na kurejesha kila senti waliyoiba. Hapa nakumbuka kilichowapata wahujumu uchumi na walanguzi katika miaka ya 80 wakati Marehemu Edward Sokoine (waziri mkuu wa zamani) angali hai.&lt;br /&gt;Hatua ya pili ije kwa washirika wao, yaani wanasiasa waongo. Hao wanaotudanganya eti hatuibiwi, hao wanaosingizia mambo mengine eti ndio sababu kuu za umasikini wetu, kumbe sivyo. Hukumu ya hawa iliyorasmi ianzie katika chaguzi ndogo zinazojitokeza. Hatimaye kiama chao kije mwaka 2010.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tutakapoingia katika uchaguzi mkuu wa 2010, twende kwenye vituo vya kura kupiga kura dhidi ya UMASIKINI, dhidi ya WIZI, dhidi ya UONGO, dhidi ya UFISADI, dhidi ya TAKRIMA na mama yake RUSHWA, tena dhidi ya tuliowapa dhamana WAKATUSARITI.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwaka huo tutaziba masikio yetu dhidi ya sera za ulaghai, tutapenda kusimsikiliza atakayetuambia ushiriki wake katika kutuibia au katika kupambana na wizi nchini (yaani chanzo kikuu cha ufukara wetu) Hatafurahi akituambia atatupatia mishahara minono na tutafanya ‘prakitiko’ mwezini, bali tutampenda akizungumzia uaminifu na uadilifu wake katika kutumia kodi tunazolipa kupitia mishahara na manunuzi ya bidhaa kwa ajili ya kuboresha huduma za jamii. Tutampenda kwa sababu nchi za wenzetu wanatumia kodi kwa uadilifu kabisa, kuboresha elimu, afya, miundombinu ya usafiri, mawasiliano na nisati. Wameweza wao, na yeye hatuambie tutaweza kwa kuwa hatakuwa mshirika wa WEZI na akishirikiana nao hata kwa bahati mbaya, atajiuzulu mara moja bila kusubiri kamati Fulani imtaje, na kama pana tuhuma yuko tayari kujibu mashtaka.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Juzi tu niliambiwa na rafiki yangu mmoja raia wa Finland, kwamba asilimia sitini ya mshahara wake wa mwezi (30%) inakatwa kwa ajili ya kodi. Akasema haimuumizi na wala halalamiki kwa kuwa anajua inakoenda inafanya kazi yake barabara. Mwenzenu nilipigwa na butwaa! Nikiwa bado siamini alichosema, rafiki yetu tuliyekuwa naye karibu (yeye anatoka Canada) akachangia hoja kwa kusema nchini kwao, baada ya muda fulani, serikali huwarejeshea wafanyakazi sehemu ya makato yao ya kodi, kwa kuwa inakuwa imezitumia fedha za kodi katika kuzalisha na imekwisha kupata faida tosha kwa ajili ya majukumu yake ya kuihudumia jamii katika kipindi husika. Ndugu zangu, wenzetu hawa, hata asiye na kazi ana posho ya kila mwezi!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hatutampenda mgombea atakayetuambia yeye binafsi ataleta maisha bora kwa kila mtanzania hata aliyeko jela, maana huo ni uongo. Tutamsikiliza akija na mikakati inayotekelezeka ya kuhakikisha madini yetu hayaibiwi, Benki kuu haiwi pango la wanyang’anyi na kodi zetu zinaenda kunakotakiwa, na juhudi zetu zinatunufaisha sote sio wanajinufaisha nazo waongo, wazandiki na WEZI.&lt;br /&gt;Kura yetu ya kuanzia mwaka huo, natamani isiangalie tena habari ‘rangi’ ya chama wala uzuri wa sura ya mtu wala kiasi cha fulana, vitenge na kofia alizogawa bure wakati wa kampeni, bali tutapiga kura tukiangalia ni wapi tunataka taifa letu lielekee kimaendeleo.&lt;br /&gt;Kura yetu itekuwa imelenga kukomesha rushwa mahakamani, mizaha bungeni na uzembe serikalini. Hali kadhalika italenga kutokomeza upuuzi katika taasisi zote za umma na katika jamii kwa ujumla.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hoja yangu ndugu zanguni; Taifa letu limeibiwa sana na hiyo ndio sababu kubwa ya umasikini wetu. Ni jukumu letu sote kuacha ubinafsi, tushirikiane katika kuukomesha wizi huu, na kwa njia hiyo tutaukomesha umasikini. Hatua hiyo iende sambamba na harakati nyinginezo ndogondogo na kubwa za kuupiga vita umasikini. Lengo letu liwe moja tu, kuifanya jamii ya Tanzania inufaike na ifurahie utajiri aliotujalia mwenyezi Mungu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mungu ibariki Tanzania, utuwezeshe kushinda vita vyetu dhidi ya wezi unaoendelea kuwafunua mbele ya macho yetu, AMEN.&lt;br /&gt;.&lt;/div&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/6014809184859864743-4862435991038001183?l=georgekahangwa.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://georgekahangwa.blogspot.com/feeds/4862435991038001183/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=6014809184859864743&amp;postID=4862435991038001183' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/6014809184859864743/posts/default/4862435991038001183'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/6014809184859864743/posts/default/4862435991038001183'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://georgekahangwa.blogspot.com/2008/02/chanzo-kikuu-cha-umasikini-wa-tanzania.html' title='CHANZO KIKUU CHA UMASKINI WA TANZANIA'/><author><name>Kahangwa</name><uri>http://www.blogger.com/profile/07414631690002879283</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='32' height='24' src='http://bp3.blogger.com/_3R2qky2qHsg/R9AwRuFfYjI/AAAAAAAAAAM/4OhJy7kgqsE/S220/george.jpg'/></author><thr:total>0</thr:total></entry></feed>
